• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA YAANZISHA MADAWATI YA SEKTA BINAFSI KILA HALMASHAURI.

Posted on: April 17th, 2017

Mkoa wa Singida umeanzisha madawati ya sekta binafsi katika halmashauri zake saba za Mkoa ili kuratibu changamoto na fursa zilizopo katika kuboresha sekta binafsi kwakuwa zimekuwa zikichangia uchumi wa taifa kwa kiasi kikubwa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya viongozi na wawezeshaji wa baraza la uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kanda ya kati ikijumuisha mikoa ya Singida, Dodoma, Shinyanga, Simiyu na Shinyanga.

Dkt. Nchimbi amesema sekta binafsi zimekuwa zikitoa huduma kwa wananchi na kuongeza uchumi wa taifa hivyo serikali inapaswa kuwezesha uboreshaji wa mazingira ili zifanye kazi kwa ufanisi.

Aidha amesema katika kusaidia sekta binafsi zilizopo mkoani Singida, halmashauri zote zimekubaliana kutangaza bidhaa na huduma zitolewazo na sekta hizo ili zipate fursa ya kujulikana na watanzania pamoja huduma na fursa za uwekezaji kwa kila halmashauri.

Amesema Mkoa wa Singida una fursa nyingi za uwekezaji katika kilimo, biashara, madini na utalii na mkoa wa Singida si masikini wala kame kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidhani.

“Singida hakuna ukame, mahindi yana stawi vizuri, alizeti tunastawisha kwa wingi sana, vitunguu vizuri vinastawi kwa wingi, tuna fuga kuku wazuri wa kienyeji ambao hawaishi na husambazwa kote nchini, tuna madini ya dhahabu na aluminium, mtu akisema Singida ni kame na masikini nadhani anakosea kabisa” ameongeza Dkt. Nchimbi.

Akizungumza kuhusu uwezeshaji wananchi kiuchumi Dkt. Nchimbi amesema baraza hilo litafanikiwa endapo uwezeshaji utajikita zaidi katika kutoa elimu na kubadilisha wananchi kifikra ili waendane na kasi ya kuchapa kazi na kuwa wabunifu.

Naye mwenyekiti wa baraza la uwezeshaji Taifa, Dkt. John Jingu amesema lengo la kuanzishwa kwa baraza hilo ni kuwezesha wananchi wote wanashiriki kikamilifu katika kuchangia ukuaji wa uchumi nchini.

Dkt. Jingu amesema baraza litajikita katika kuboresha kilimo hasa cha umwagiliaji na upatikanaji wa masoko ya nafaka zinazozalishwa na wakulima na kuboresha ufugaji ili uwe wa kisasa.

Mafunzo kwa viongozi na wawezeshaji wananchi kiuchumi kutoka mikoa ya Singida, Dodoma, Manyara, Shinyanga na Geita yamefanyika Mjini Singida katika ukumbi wa Veta ambapo wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi na maafisa wawezeshaji kutoka mikoa hiyo wameshiriki.

Matangazo

  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 - MKOA WA SINGIDA December 18, 2020
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2019/2020 SINGIDA RS - GPN 2019 - 2020 August 23, 2019
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2018/2019 September 15, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA AWATAKA WAZAZI, MAAFISA USTAWI KUWA KARIBU NA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    December 31, 2020
  • TAKWIMU ZAIVUSHA TANZANIA UCHUMI WA KATI- DKT. LUTAMBI

    November 01, 2020
  • UN YAMUUNGA MKONO MAGUFULI KUTOKOMEZA UKATILI WA MWANAMKE IKUNGI

    October 23, 2020
  • VIONGOZI WA DINI SINGIDA WATOA MAAZIMIO MAZITO SABA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    October 22, 2020
  • Angalia Zote

Video

Baraza la hoja Mkalama 2017
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.