• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

Posted on: February 1st, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amewataka wananchi wa Mkoa wa Singida kuwekeza zaidi katika kilimo cha alizeti kutokana na fursa kubwa ya uzalishaji inayopatikana katika mkoa huo pamoja na udongo wake kuwa na rutuba inayofaa kwa zao hilo.

Akizungumza leo katika kijiji cha Mnang’ana, kata ya Sepuka, Wilaya ya Ikungi, Mhe. Dendego amesema alizeti ni zao la kimkakati kwa mkoa huo kwani linaweza kuwa chanzo kikubwa cha kipato kwa wakulima na kuchangia ukuaji wa uchumi wa mkoa.

Akijibu swali la mdau kuhusu mkakati wa mkoa katika kuhakikisha upatikanaji wa mazao bora ya alizeti, Mkuu wa Mkoa amesema kupitia sekta ya kilimo, mkoa umeandaa mbegu bora za alizeti chotara zenye ustahimilivu na uwezo wa kutoa mavuno makubwa.

“Tunawahimiza wakulima kuchangamkia fursa hii kwa kutumia mbegu bora tulizozitayarisha, kwani zitasaidia kuongeza uzalishaji, kipato na kuboresha maisha ya wananchi,” amesema Mhe. Dendego.

Kadhalika,Katika hotuba hiyo, Mhe. Dendego amesisitiza umuhimu wa wazazi na walezi kutoa malezi bora kwa watoto wao ili kukabiliana na changamoto ya mmomonyoko wa maadili unaoendelea kushuhudiwa katika jamii.

Amesema wazazi wanapaswa kuwafuatilia watoto wao kwa karibu, kuwalea kwa misingi ya maadili mema, na kuhakikisha wanapata malezi bora yanayojumuisha elimu ya darasani pamoja na malezi ya kiutu na kiutamaduni.

“Wazazi mna jukumu kubwa la kuhakikisha watoto wetu wanakua katika maadili mema, wanaheshimu mila na tamaduni za Kitanzania, na kuwa raia wema wa kesho,” amesisitiza.

Hayo yalijiri wakati Mhe. Dendego aliposhiriki katika zoezi la upandaji wa miti lililoandaliwa na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Tanzania kupitia BAKWATA Mkoa wa Singida, ambapo alipanda mti wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika eneo la Msikiti wa Mnang’ana pamoja na Shule ya Msingi Mnang’ana.

Katika zoezi hilo, viongozi wa dini walihimiza jamii kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda na kutunza miti, wakisisitiza kuwa kufanya hivyo ni sehemu ya ibada na mchango muhimu katika kulinda uhai wa binadamu.



Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • MAAFISA UGANI WAASWA KUWA WATATUZI KERO ZA WAKULIMA SHAMBANI

    February 02, 2026
  • TSH. 27,000/- PEKEE KUWASHA UMEME KILA KAYA.

    February 03, 2026
  • SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

    February 01, 2026
  • "KILA MMOJA ALINDE ENEO LAKE NA KUFUATA SHERIA" - RC DENDEGO

    January 27, 2026
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.