• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Miradi ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa, Hospitali na visima vya maji kukamilishwa kabla ya Desemba 10, 2021 - RC SINGIDA

Posted on: November 8th, 2021

Bodi za shule za msingi na sekondari pamoja na Madiwani katika kata mbalimbali mkoani Singida wametakiwa kuwashirikisha wananchi katika Ujenzi wa vyumba vya madarasa, Hospitali na visima vya maji ili kukamilisha Ujenzi huo kabla ya Desemba 10, 2021.

Mkuu wa Mkoa Singida Dkt. Binilith Mahenge  ametoa kauli hiyo leo tarehe 8.11.2021 alipotembelea Ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Manyoni iliyopo wilayani humo na kukuta wafanyakazi na  mafundi wachache jambo ambalo halikumfurahisha.

"Katika Wilaya nyingine wananchi wamehamasika ambapo walichimba msingi na kusaidia kusogeza mchanga  kokoto na zege  na kusaidia kufanya kazi kwenda kwa haraka, sasa hapa kuna mafundi watatu hawawezi kumaliza kazi hii kwa wakati.” Alisema Dkt.Mahenge

Dkt Mahenge amesema Mpango uliopo ni kuhakikisha vyumba 662 vya madarasa kwa sekondari na Msingi shikizi kwa mkoa kukamilika kabla ya Decemba 15 mwaka huu na endapo kazi hiyo itashindikana kukamilishwa kwa namna yoyote ile wasimamizi wanaohusika waajiandae kufukuzwa kazi.

Hata hivyo amezitaka Bodi za shule kuhakikisha kwamba wanawashirikisha wananchi katika Ujenzi huo na kuacha kudhani kwamba hela hizo zitatosha kwa kila kitu.

Aidha amesema wadau wanaruhusiwa kuchangia  baadhi ya vitendea kazi ikiwemo mchanga, kokoto au nguvu kazi kwa kuwa  kila darasa lilikadiriwa kutumia kiasi cha sh.Milion 20 kwa kila darasa.

Amemtaka Mkurungezi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kuhakikisha wananunua vifaa kwa pamoja ili kupunguza gharama ikiwa ni pamoja na kutoa Oda mapema kwa kuwa mahitaji ni makubwa ambapo kila mkoa vinahitajika.

"Nataka mjiongeze hakutakuwa na msamaha kwa yeyote atakayesababisha wanafunzi kukosa madarasa wakati hela tayari zimeshatolewa, sitahitaji kusikia eti vifaa viliisha, ndio maana nasema mjiongeze mtoe oda mapema."Alikaririwa Mkuu wa Mkoa.

Naye Alhaji Juma Kilimba Mwenyekiti wa CCM Mkoa akawataka viongozi wote wa chama Mkoa, Kata na tarafa kuhakikisha wanasimamia na kuhimiza wananchi kushiriki nguvu kazi ili kuhakikisha kwamba wanafunzi wote wanapata madarasa ifikapo tarehe 15 Desemba mwaka huu.

Pia amewataka mafundi wote mkoani hapo waliochaguliwa kufanya kazi hizo kuongeza idadi ya mafundi na vibarua ili kazi zisikwame na ziweze kukamilika kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya hiyo Rahabu Magesa, akasisitiza kwamba wamejipanga kutembea mashule yote ambayo wanaendelea na Ujenzi wa vyumba vya  madarasa ili kusimamia na kuhakikisha zoezi linafanikiwa kama ilivyopangwa.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.