• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

CCM SINGIDA YATAKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO KUIMARIKA.

Posted on: August 16th, 2021

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Mhe.  Juma Kilimba amewataka viongozi wa miradi mbalimbali mkoani hapo kuongeza juhudi katika usimamizi  wa miradi wanayoitekeleza ili kulinda thamani ya fedha za Serikali  zinazotumika kukamilisha  miradi hiyo.

Akiongea leo tarehe 16/8/2021 wakati wa kuhitimisha ziara yake  kwa wilaya ya Iramba katika ukumbi wa Halmashauri hiyo  Mhe. Kilimba  amewapongeza viongozi hao kwa hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi na  kuwataka kushughulikia baadhi ya changamoto ndogo ndogo walizozibaini  katika  miradi sita waliyoitembelea.

Miradi iliyotembelewa na Mwenyekiti wa CCM mkoa ni ile inayohusiana na ukarabati na ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Tumaini, ujenzi wa darasa moja  katika shule ya msingi  Ulyang’ombe,  ujenzi wa zahanati moja (OPD),  Matengenezo ya barabara  kutoka Shelui  kupita  Mtoa hadi Ndago, mradi mwingine ni ule wa  umeme wa ujazilizi  katika vitongoji vya Pangani na Kintende pamoja na mradi wa miche ya miti katika eneo la Lulumba.

“Ujenzi wa Hospitali kata ya Mkunda  iliyogharimu shilingi milioni 50, umaliziaji wa chumba cha darasa katika shule ya msingi Ulyango’ombe, ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 30.74 inayogharimu kiasi cha milioni 199.9, mradi wa umeme na ujenzi wa mabweni  katika shule ya sekondari Tumaini na mradi wa huduma za misitu ni miradi ambayo imekuwa na faida kubwa kwa wananchi wa Iramba, tuhakikishe inakamilika kwa wakati na kwa viwango vilivyotarajiwa na Serikali.” Alisema Juma Kilimba

Amewataka viongozi wanaosimamia miradi hiyo  kuongeza umakinifu  katika usimamizi wa miradi pamoja matumizi sahihi ya fedha za Serikali  ili kufikia lengo la kuwasogezea huduma wananchi kwa ukaribu.

Aidha, Mhe, Juma amewapongeza wanachi wa wilaya ya Iramba kwa kujitokeza kwa hali na mali katika kuchangia ujenzi wa hospitali na shule mbalimbali wilayani hapo na kuwataka wananchi wa wilaya za jirani kuiga ushiriki wa shughuli za maendeleo badala ya kuiachia Serikali .

Mkandarasi wa kampuni ya M/S chase investment group ltd ya mkoani Mwanza inayosimamia ujenzi wa barabara hiyo,  amesema ujenzi umegharimu kiasi cha shilingi 199,917,000 ikihusisha kuchonga barabara km 30,74 Kuweka changarawe km 13, ukarabati  wa makalavati saba (7) na ujenzi wa makalavati mapya  mawili  (2) pamoja na kuchimba mifereji ya maji ya mvua  yenye urefu wa mita  2694.5.

Ziara hiyo wilayani Iramba imewahusisha baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa, RC ambaye aliwakilishwa na DC Mhe. Paskasi Muragili pamoja na DC wa  Iramba Mhe. Suleimani Mwenda na wakuu wa Idara mbalimbali.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

 Mradi wa ujenzi wa mabweni  katika shule ya sekondari Tumaini

Mradi wa miche ya miti katika eneo la Lulumba 

http://singidars.blogspot.com

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.