• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Chongolo atoa maagizo mazito kwa TRA

Posted on: February 27th, 2023

Katibu Mkuu CCM Daniel Chongolo ameagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakisha wanatoa cheti cha msamaha wa kodi wa ongezeko la thamani (VAT) kwa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kabla ya kumaliza ziara yake ili Mkandarasi wa Mradi wa Maji unaotekelezwa katika Kata ya Chikuyu Wilayani Manyoni Mkoani Singida aweze kukamilisha kazi hiyo.

Kauli hiyo ameitoa leo wakati alipotembelea Mradi huo baada yakupata maelezo ya utekelezaji wa Mradi kutoka kwa Meneja wa RUWASA Mkoa Said Lukas, kwamba wanasubiri cheti hicho ili Mkandarasi aweze kuendelea na kazi, Cheti ambacho kingekamilika kwa muda wa wiki mbili hadi tatu zijazo.

Katibu Mkuu alieleza kwamba chama hakiwezi kuvumilia ucheleweshaji wa ukamilishwaji wa miradi ambayo wananchi wanauhitaji mkubwa kwa sababu ya watu wachache ambao hawakamilishi wajibu wao.

"Hatuwezi kuwa tunajadili vitu vidovidogo ambavyo havihitaji fedha kuvichukulia hatua na kuvitekeleza, hivi inaonesha kuna watu wapo katikati hawataki kutimiza wajibu wao na sisi hatupo tayari tunachotaka nikutoa huduma ya maji kwa wananchi" alisema Chongolo na kuongeza

"Tunajadili swala la certificate wakati Wizara ya Maji na TRA wote wanatumia Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, sasa nataka kabla sijaondoka Singida certificate iwe imefika" alimalizia Chongolo.

Hata hivyo Chongolo amemuelekeza Meneja huyo kuhakikisha vijiji vilivyopitiwa na bomba hilo kuhakikisha vinapatiwa maji.

Awali akitoa ufafanuzi wa taarifa ya mradi Said Lukas, alieleza kwamba mradi huo ukikamilika utagharimu Bilioni 12 na utafikia vijiji 11 vya Wilayani Manyoni.

Amesema Mradi huo ulianza Julai 2017 na unategemewa kukamilika Desemba 2023 na inategemewa kuwafikia wananchi zaidi ya Elfu 55 ambapo mpaka sasa jumla ya Bilioni 4.9 zimekwisha tumika.

Aidha amesema kwamba Mradi huo utakapo kamilika utaongeza hali ya upatikanaji wa maji kutoka asilimia 54 mpaka kufikia asilimia 84.

Hata hivyo Katibu Mkuu huyo atafanya ziara Mkoani Singida kwa muda wa siku sita (6) ambapo atakagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule, vituo vya afya, barabara, miradi ya maji pamoja na kuzungumza na wananchi.

Mwisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.