• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

CRDB IWASAIDIE VIJANA WAWEZE KUTUMIA FURSA ZILIZOPO; WASIONE FAHARI KUJIITA ‘MABOMU’.

Posted on: October 3rd, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ameishauri Benki ya CRDB Mkoa wa Singida kuwasiadia vijana elimu na mikopo ya kutambua na kutumia fursa zilizopo ili waachane na kauli za kujiita ‘mabomu yanayosubiri kulipuka’.

Dkt Nchimbi ametoa ushauri huo mapema leo wakati akizindua wiki ya huduma kwa mteja katika benki ya CRDB tawi la Singida huku akisisitiza benki hiyo kuwa bega kwa began a Vijana.

“Vijana wetu wasione fahari kabisa kujiita mabomu yanayosubiri kulipa, Singida tuna fursa nyingi wasibweteke watumie benki hizi na nyinyi pamoja na benki nyingine jitahidini kuwashika vijana hawa wakipewa elimu ya ujasiriamali na mikopo wataifikisha Singida mbali kiuchumi”, amesema Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Singida umejipanga kuzalisha chakula cha kutosha ili uweze kulisha makao makuu ya nchi yaani Dodoma hivyo vijana wabadilike na wawe mabomba ya kusafirishia chakula na bidhaa mbali mbali.

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa huduma za kibenki zinawasaidia watumishi wa umma katika kupanga matumizi ya pesa kwakuwa isingekuwa mishahara kupitia benki kungekuwa hakuna kinachosalia katika mishahara yao huku hicho kidogo kinachosalia kinakuwa cha muhimu sana.

Ameongeza kuwa kuelekea uchumi wa kati na Tanzania ya viwanda huduma bora za kibenki ni hakikisho la safari hiyo kuwa salama na yenyewe uhakika huku benki zikiwa ni  mahali panapo waunganishawajasiriamali wakubwa kwa wadogo.

Ameongeza kuwa benki ya Crdb inaaminika ndio maana wajasiriamali na watumishi wengi wamekuwa wakiitumia hivyo na wateja wao pia wajenge tabia ya kuaminika hasa kwa kurejesha mikopo yao bila usumbufu.

“Watu wengi wamekuwa wakikopa bila ya kuwa na malengo hivyo kuishia lawama au hukopa kwa mazoea bila ya kujiandaa nini atafanyia huo mkopo, mteja wa hivyo anaweza kubadilika na kutokuwa mwaminifu hivyo benki mna jukumu kubwa la kutoa elimu ya kutosha wateja wenu”, amefafanua Dkt Nchimbi.

Ameeleza kua benki iendelee kuwaelimisha wajasiriamali na wananchi wengine kuwa kukopa sio aibu na mtu ambaye anakopesheka hiyo ni heshima hivyo atambue fursa hiyo na kuitumia vizuri.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya CRDB Singida Innocent Arbogast ameeleza kuwa benki hiyo inatoa mikopo kuanzia kwa wajasiriamali wadogo mpaka wakubwa pamoja na kutoa elimu pamoja na huduma za Sim banking, malkia akaunti na akaunti za watoto.

Arbogast amesema kuwa wiki ya huduma kwa mteja wataitumia vizuri kwa kuwatembelea wajasiriamali wote mitaani na kuelezea huduma zao kwakuwa wiki ya huduma kwa mteja ina lenga kuongeza uaminifu kati ya benki na wateja wao.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora Magiligimba amesema benki hiyo imekuwa ikiwasaidia watumishi ili waweze kutimiza malengo yao huku watumishi wakiwa waaminifu katika kurejesha mikopo hiyo.

ACP Magiligimba ametoa mfano wake yeye ambaye ameweza kujenga nyumba kutokana na mkopo wa benki hiyo hivyo watumishi wengine wasione aibu kukopa ila wawe wamejiwekea malengo mazuri ya matumizi ya mikopo hiyo.

Meneja wa Benki ya CRDB Singida Innocent Arbogast akijiandaa kumlisha keki Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi wakati wa kuzindua wiki ya huduma kwa mteja katika benki hiyo.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.