• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DC MURAGILI AWATAKA WATENDAJI KUTUMIA MATOKEO YA SENSA 2022 KATIKA KUWEKA MIPANGO BORA YA MAENDELEO.

Posted on: July 9th, 2023

VIONGOZI na watendaji wa Halmashauri za Wilaya ya Singida wametakiwa kuweka mipango na mikakati bora ya maendeleo inayoendana na kiwango cha ongezeko la idadi ya watu katika maeneo yao iliyotokana na matokeo ya Sensa ya mwaka huu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 katika Wilaya ya Singida yaliyofanyika tarehe 8 Julai, 2023 kwenye ukumbi wa Sekondari ya Mwenge iliyopo Singida mjini Mkuu wa Wilaya hiyo Mhandisi Paskasi Muragili, amesema ongezeko la idadi ya watu iwe ni chachu ya maendeleo.

DC Muragili amesema Halmashauri zinatakiwa kuweka mipango bora ya kuwaendeleza na kuendeleza uzalishaji katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, afya, elimu, miundombinu, uchumi ili kukabiliana na ongezeko la idadi ya watu.

“Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya watu katika Halmashauri zetu zote mbili inazidi kuongezeka, hivyo kupitia mafunzo haya ni wajibu wa sisi viongozi na watendaji wote kwenda kupanga mipango thabiti”. Mhandisi Muragili   

Amesisitiza kuwa wananchi wakiwa na uelewa mzuri wa matumizi ya matokeo ya Sensa ya watu na makazi itasaidia kutoa mchango wao katika maendeleo ya Taifa kwa kuwa watakuwa  na uwezo sio tu wa kuishauri Serikali bali pia kupima utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya nchi na maeneo yao wanamoishi.

Katika hatua nyingine DC Muragili amepongeza juhudi za viongozi wa Wilaya ya Singida kwa kuwa maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24 ya Halmashauri ya Manispaa na Singida DC yamezingatia matumizi ya matokeo ya Sensa na tafiti nyingine za kitakwimu zinazozalishwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

DC Muragili amehitimisha hotuba yake kwa kusema kuwa matumizi bora ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi, Majengo na Anwani ya Makazi ya Mwaka 2022 yataongeza umakini na ufanisi katika kutekeleza majukumu Serikalini na katika sekta Binafsi hivyo kuharakisha maendeleo kwa wananchi wa Singida.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga ametoa wito kwa waratibu wa Sensa wa Halmashauri za Wilaya mkoani Singida kusambaza matokeo ya Sensa ya mwaka huu katika ofisi zao ili takwimu hizo zianze kutumika hususan katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa maeneo husika.

Dkt. Mganga amesema Mkoa wa Singida umejipanga kuhakikisha mipango na programu zote za maendeleo zinapangwa kwa kuzingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi, Sensa ya Majengo na Sensa ya Anwani za Makazi ya Mwaka 2022.

“Tumejipanga kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki kwa wakati na zenye ubora unaozingatia mahitaji halisi ya wananchi kulingana na idadi yao, jinsi yao, kuzingatia mahitaji maalum ya makundi mbalimbali katika jamii na hali ya mazingira wanamoishi” Dkt. Fatuma Mganga

Mkoa wa Singida kutokana na matokeo ya Sensa ya mwaka 2022 una idadi ya watu 2,008,058 kutoka watu 1,370,637 mwaka 2012 kati ya idadi hiyo watu 995,703 ni wanaume na watu 1,012,355 ni wanawake. Hivyo inaonyesha kiwango cha ukuaji wa idida ya watu imeongezeka katika kipindi cha miaka kumi iliyopita kwa wastani wa asilimia 3.8 kikiwa zaidi ya wastani wa taifa ambao ni 3.2

Meneja Takwimu Ofisi ya Taifa ya Takwimu Mkoa wa Singida Naing'oya Kipuyo akisoma hotuba kwa niaba ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa viongozi na watendaji wa Wilaya ya Singida ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili, yaliyofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Mwenge Singida mjini tarehe 08 Julai 2023






Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.