• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DINI NI NYENZO YA MAADILI, UMOJA NA UTIIFU WA SHERIA – DKT. FATUMA MGANGA

Posted on: February 8th, 2026

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amesema taasisi za dini ni nguzo muhimu katika kujenga maadili, kuimarisha umoja wa kitaifa na kukuza utii wa sheria miongoni mwa wananchi, akisisitiza kuwa maendeleo ya taifa yanahitaji jamii yenye hofu ya Mungu.
Dkt. Mganga alitoa kauli hiyo alipokuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia ununuzi wa vyombo vya muziki vya Kanisa la EAGT Nduguti, Wilaya ya Mkalama, yenye lengo la kukusanya Shilingi milioni 15. Alieleza kuwa vyombo hivyo vitatumika kuimarisha ibada, mafundisho ya kiroho na semina zitakazochangia mabadiliko chanya ya kijamii.


Alifafanua kuwa hofu ya Mungu hujengwa kupitia malezi na mafundisho yanayotolewa na taasisi za dini, hali inayosaidia kupata raia watiifu, wanaozingatia sheria na kuepuka vitendo vya rushwa, ufisadi na uhalifu. Alisisitiza kuwa jamii yenye misingi imara ya kiroho ni msingi wa utawala bora na amani ya kudumu.

Aidha, Dkt. Mganga alisema shughuli hiyo imeonesha mshikamano wa kijamii kwa kuwakutanisha wananchi wa imani tofauti kushiriki lengo moja la maendeleo. Alieleza kuwa ushiriki wa viongozi wa Serikali, viongozi wa dini na wananchi kwa pamoja unaimarisha umoja na ushirikiano unaohitajika katika kujenga taifa lenye maadili.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkalama, Bi. Happyness Sulle, alisema taasisi za dini zimekuwa washirika wakuu wa Serikali katika kuhubiri amani, maadili na mshikamano, hususan kwa vijana, jambo linalochangia utulivu na maendeleo ya wilaya hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Bi. Asia Messos, alisema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za dini katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo, akibainisha kuwa maendeleo ya jamii yanahitaji ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na taasisi za dini.

Akizungumza kwa niaba ya Kanisa la EAGT Nduguti, Mchungaji wa Kanisa hilo alisema taasisi za dini zitaendelea kuwa mstari wa mbele katika kukuza maadili mema, kupunguza vitendo vya uhalifu na kuijenga jamii yenye hofu ya Mungu kwa kushirikiana na Serikali.Harambee hiyo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha ibada, malezi ya kiroho na mshikamano wa kijamii, kwa lengo la kujenga taifa lenye maadili, umoja na utii wa sheria.


https://www.youtube.com/watch?v=M7aatIDpxbI&pp=ygUJU2luZ2lkYXJz 

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DINI NI NYENZO YA MAADILI, UMOJA NA UTIIFU WA SHERIA – DKT. FATUMA MGANGA

    February 08, 2026
  • RC DENDEGO ASISITIZA USHIRIKIANO WA SERIKALI NA WADAU WA KILIMO.

    February 06, 2026
  • MAAFISA UGANI WAASWA KUWA WATATUZI KERO ZA WAKULIMA SHAMBANI

    February 02, 2026
  • TSH. 27,000/- PEKEE KUWASHA UMEME KILA KAYA.

    February 03, 2026
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.