• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Diwani atajwa kuchafua hali ya hewa Mitundu, RC Serukamba amvutia kasi.

Posted on: June 7th, 2023

Wananchi  na Diwani wa kata ya Mitundu Katika Halmashauri ya Itigi Wilayani Manyoni Mkoani Singida Patrick  Masanja  wamelalamikiwa na viongozi wa Serikali kukataa kushiriki nguvu kazi katika miradi ya  maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa  na Kituo cha Afya eneo hilo kwa sababu ambazo hazikuweza kufahamika mara moja.

Malalamiko hayo yametolewa leo na  Viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya hiyo Kemilembe Lwota mbele ya Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba kwamba wananchi wamekuwa wakikatazwa na Diwani huyo kushiriki nguvu kazi katika miradi  ya ujenzi wa madarasa na Kituo cha Afya cha kata hiyo jambo ambalo limesababisha gharama na muda wa ujenzi kuongezeka.

DC Kemilembe alisema siku za karibuni walitembelea miradi hiyo na kamati ya usalama ya Wilaya na Diwani huyo alikataa kushiriki ziara hiyo kwa kuwa malalamiko yalikuwa mengi dhidi yake kuhusu kuwakataza wananchi wa eneo hilo kushiriki ujenzi wa miradi.

Hata hivyo kamati ya siasa ya Wilaya nayo iletembemea eneo hilo na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi ambapo DC Kemilembe amesema walimpatia nafasi Diwani huyo kuwaeleza wananchi hao kushiriki nguvu kazi katika miradi hiyo na alikataa kuongea neno lolote.

Naye Mwemwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Manyoni Barnabas Moshi alieleza kwamba Diwani huyo amekuwa ni changamoto eneo hilo ambapo kamati ya siasa ilipopata malalamiko dhidi yake walikuja kufanya mkutano na wananchi na hakuonesha ushirikiano.

Aidha kwa upande wake Diwani huyo alijitetea kwamba ni kweli wananchi hao hawashiriki kwenye ujenzi wa miradi hiyo kwa sababu wanazozijua wao wenyewe lakini yeye hajawakataza huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi akimhakikishia RC Serukamba kwamba mara kadhaa Diwani huyo amekuwa akiwakataza wananchi kufanya kazi katika Kituo cha Afya cha Mitundu.

Akimalizia mjadala huo Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa Halmashauri kuongeza idadi ya mafundi na vibarua katika miradi hiyo ili miradi ikamilike ifikapo tarehe 20/6/2023 huku akiahidi bàadhi ya wananchi na waliokuwepo eneo hilo kwamba swala la Diwani huyo anaenda kutafakari ili kujua jambo la kufanya dhidi yake.

 Hata hivyo RC Serukamba ametoa pongezi kwa Wilaya kwa hatua ambayo miradi hiyo imefikiwa huku akiwasisitiza kukamilisha ifikapo tarehe 20/06/2023 na kuwataka kuhakikisha zahanati na vituo vya Afya kuanza kutoa huduma kwa wananchi ifikapo 1/7/2023.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.