• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DKT. FATUMA MGANGA AONGOZA KAMPENI YA UPANDAJI MITI NA UKAGUZI WA MIRADI IKUNGI

Posted on: January 27th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi leo tarehe 27 Januari, 2025, ikiongozwa na Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, imezindua kampeni ya upandaji miti chini ya kauli mbiu isemayo “Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti,”

ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Zoezi hilo la upandaji miti limefanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Ikungi na Shule mpya ya Msingi Mshikamano, ambapo watumishi wa Halmashauri, walimu pamoja na wanafunzi kutoka shule za msingi na sekondari za Unyahati walishiriki kikamilifu, na zaidi ya miti 200 ilipandwa.

Akizungumza katika tukio hilo, Dkt. Mganga alisisitiza kuwa kampeni hiyo ni sehemu ya mkakati wa Halmashauri wa kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Kwa msimu wa mwaka 2025/2026, Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi inatarajia kupanda jumla ya miti 1,500,000 ya aina mbalimbali ikiwemo ya matunda, kivuli na mbao, kwa kushirikiana na wadau wa mazingira waliopo wilayani.

Hadi sasa, Halmashauri imefanikiwa kusambaza miche ya miti 3,200 katika maeneo mbalimbali ya wilaya, ikiwemo Shule ya Msingi Puma na Kijiji cha Mnangana kilichopo katika Tarafa ya Sepuka.

Baada ya uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti, Dkt. Mganga aliendelea na ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo leo tarehe 27 Januari, 2026, katika kata za Misughaa, Puma na Unyahati, kwa lengo la kujiridhisha na maendeleo ya utekelezaji wa miradi na kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Katika Kata ya Misughaa, alikagua ujenzi wa Kituo cha Afya kinachogharimu Shilingi milioni 250, ambacho kipo katika hatua ya upauaji, na kinatarajiwa kukamilika mwezi Februari.

Katika Kata ya Puma, alitembelea Shule ya Msingi Puma B inayogharimu Shilingi milioni 545.4, ambapo aliagiza kuongezwa kwa idadi ya mafundi ili kuhakikisha mradi unakamilika kabla ya tarehe 15 Februari 2026.

Ziara hiyo ilihitimishwa katika Shule ya Mshikamano iliyopo Kata ya Unyahati, mradi unaogharimu takribani Shilingi milioni 302.2, unaotekelezwa kupitia Mpango wa BOOST kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, na upo katika hatua za mwisho za ukamilishaji.

Akihitimisha ziara hiyo, Dkt. Fatuma Mganga amesisitiza kuwa maendeleo ya kweli lazima yaende sambamba na utunzaji wa mazingira, akibainisha kuwa miradi ya elimu na afya haina maana ikiwa mazingira hayalindwi kwa ajili ya kizazi kijacho.

Ameagiza wasimamizi wa miradi kusimamia kikamilifu ubora na muda wa utekelezaji, huku akiwaelekeza viongozi na wananchi kushiriki kwa dhati katika utunzaji wa miti iliyopandwa na matumizi ya huduma za kijamii, ikiwemo Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, ili kuhakikisha Ikungi inapata maendeleo endelevu na salama.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "WATOTO WANAOPATA LISHE WANAFABYA VIZURI DARASANI" MWL. DULENGA

    February 12, 2026
  • DINI NI NYENZO YA MAADILI, UMOJA NA UTIIFU WA SHERIA – DKT. FATUMA MGANGA

    February 08, 2026
  • RC DENDEGO ASISITIZA USHIRIKIANO WA SERIKALI NA WADAU WA KILIMO.

    February 06, 2026
  • MAAFISA UGANI WAASWA KUWA WATATUZI KERO ZA WAKULIMA SHAMBANI

    February 02, 2026
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.