• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Dkt. Mganga ataka uwajibikaji katika kuinua ufaulu katika shule za msingi mkoani Singida

Posted on: May 17th, 2023

Maafisa Elimu  wote na Wakuu wa shule mkoani Singida wametakiwa kutumia mbinu mbalimbali kusimamia taaluma ili  kuhakikisha ufaulu unaongezeka katika shule za msingi.

Maelekezo hayo yametolewa leo na Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga wakati alipokutana na Wakuu wa shule na Maafisa elimu Mkoa, Maafisa elimu Wilaya, Maafisa elimu kata Mkutano uliofanyika Katika ukumbi wa mikutano ulipo katika shule ya Sekondari St. Bernard.

Akiwa katika kikao hicho RAS amewataka  Maafisa elimu kuwa watatuzi wa changamoto za Walimu ikiwa ni pamoja na kuzitembelea shule na kuja na mikakati ya kuboresha elimu kwa kuhakikisha kila mwalimu anatimiza majukumu yake na kufanya kazi kwa ushindani.

Ameagiza wakuu wa shule kuwa na kawaida ya kufanya tathimini ya  kila wiki kwa walimu na masomo wanayo yafundisha ili kubaini mapungufu na namna ya kutatua  ambapo amesema itasaidia kuwapima kutokana na matokeo.

Dkt. Mganga amesema ni wakati sasa walimu hao pamoja na watendaji wengine wakiwemo maafisa elimu kutoka maofisi kwenda kwenye shule ambazo zinachangamoto ili kuinua hali ya elimu kwa kufanya tathmini ya wanafunzi ambao wanashindwa kuwa na matokeo mazuri.

“Twendeni tukafanye kazi, tuache ubosi, twendeni tukafanye tathmini tujue mwanafunzi gani anachangamoto ipi ili tuweze kuzikabili changamoto ambazo zinaturudisha nyuma kiwango cha elimu kwenye mkoa wetu”. Alisema Dkt. Mganga

“Kiongozi unaweka mikakati ili kuweza kupata matokeo usisikilize Rumors tumia jitihada zako upate matokeo ili uweke Legacy”. Aliongeza Katibu Tawala huyo.

Dkt. Mganga aliongeza kwa kusema kuwa viongozi wa Mkoa wa Singida wanapaswa kufanya kazi kwa kujituma ili waweze kuweka alama hivyo akasisitiza walimu wakuu kujituma na kujitoa zaidi kwenye kutoa elimu kwa wanafunzi.

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Bahi, Boniface Willson ambaye alikuja kuwajengea uwezo walimu wa mkoa wa Singida alisema kuwa mwaka 2017 Halmashauri ya Bahi ilikuwa na shule ambazo zilikuwa hazifanyi vizuri kwenye elimu msingi hadi ikapewa bendera nyeusi lakini baada ya kufanya tathimini kwa sasa imekuwa ikifanya vizuri.

Willson alisema kujituma kwa walimu wakuu kwenye Halmashauri hiyo ndiko kumeweza kubadilisha kutoka ufaulu wa chini na sasa imekuwa moja ya Halmashauri inayofanya vizuri ndani ki mkoa hadi kitaifa.

Naye Mratibu wa Programu ya Serikali ya Shule Bora Mkoa wa Singida Samweli Daniel amewashauri wadau wa elimu wanapopanga mipango ya kuboresha elimu iwe inaandikiwa ripoti ili zitumike wakati wa utekelezaji katika maeneo mbalimbali.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.