• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Halmashauri za Mkoa wa Singida zashauriwa kujenga magorofa, zapongezwa kwa usimamizi wa ujenzi wa madarasa.

Posted on: December 1st, 2022

Halmashauri za Wilaya Mkoani Singida zimeshauriwa kubadilika na kuanza kufikiria kujenga shule za ghorofa ili kuokoa maeneo ya ardhi ambayo yangeweza kutumika  kwa shughuli nyingine za maendeleo.

Ushauri huo umetolewa  leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, alipokuwa akiendelea na ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Wilaya ya Singida Vijijini, Ikungi na Manispaa.

Amesema kwa kuwa miji inapanuka kwa kasi na ardhi inakuwa ndogo hivyo ni muhimu kuanza kujenga majengo kwa  kwenda juu ili kupunguza matumizi ya ardhi.

Aidha amezipongeza Halmashauri za Singida, Ikungi na Manispaa kwa kazi nzuri ya usimamizi wa vyumba vya madarasa ambayo imefikia asilimia zaidi ya 80.

Awali akiwa katika Wilaya ya Singida amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kutumia fedha za ndani kuongeza baadhi ya vyumba vya madarasa badala ya kusubiri zinazotolewa na Serikali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Singida DC Ester Chaula,  amesema Halmashauri ya Wilaya hiyo ilipokea jumla ya  Tsh. Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 50 katika shule 17 za Sekondari.

Aidha Mkurugenzi ameeleza kwamba baada ya fedha hizo ziliwekwa katika akaunti 17 za shule hizo ambapo ameeleza kwamba kwa sasa shule hizo zipo katika hatua ya umaliziaji.

Jumla ya shilingi Milioni 581.49 zimeshatumika katika utekelezaji wa ujenzi wa madarasa hayo ambayo kwasasa madarasa hayo yamefikia asilimia 85 na wameahidi kukamilisha mpaka uwekaji wa madawati kabla ya tarehe 15 Desemba, 2022.

Aidha kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu, amesema Manispaa imepokea fedha kiasi cha Bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 50 vya madarasa ya wanafunzi wa kidato cha kwanza.

Ameendelea kusema kwamba vyumba 8 vipo katika hatua ya upakaji wa rangi, vyumba 26 vipo hatua ya skiming wakati vyumba 14 vikiwa katika hatua ya kupiga ripu na viwili (2) katika hatua ya upasuaji.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Ikungi Faraja Maluga, ameeleza kwamba Wilaya ya Ikungi imepatiwa jumla shilingi 580 Milioni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 29 katika shule 16.

Mkurugenzi huyo ameeleza kwamba madarasa hayo yote yamefikia asilimia 80 na wanategemea kukabidhi kwa muda iliyopangwa.

Mkoa wa Singida umepewa fedha jumla ya Bilioni 5.8 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 290 kwa wanafunzi wa mwaka 2023 katika Halmashauri Saba (7) za Mkoa wa Singida.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (kulia) akipokea taarifa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa mapema leo wakati wa ziara yake Singida Vijijini leo tarehe 1 Desemba, 2022. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Singida Vijijini Ester Chaula

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (kulia) akifafanuliwa jambo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida Jeshi Lupembe wakati wa ziara ya ukaguzi wa majengo ya madarasa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akiagana na viongozi mbalimbali wa Chama Tawala na Serikali wakati alipomaliza ziara yake ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madaraka katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida 1 Desemba, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (kushoto) akizungumza na kupongeza viongozi wa Wilaya ya Ikungi kwa usimamizi bora wa vyumba vya madarasa wakati wa ziara yake 1 Desemba, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro (kushoto) akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba kuhusu maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa  

Ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa Wilayani Ikungi ikiendelea

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.