• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Kamati ya Siasa Mkoani Singida Yafanya Ziara Manyoni, Itigi Watakaiwa Kukarabati Majengo Ya Zamani Ya Shule

Posted on: March 16th, 2022

Wananchi wa Mkoa wa Singida wametakiwa kuendelea kukarabati majengo ya zamani ya shule na vituo vya Afya vilivyopo mkoani hapo ili majengo hayo yaweze kuendelea kutumika kwa matumizi mbalimbali.

Wito huo umetolewa leo na Mwenyekiti  wa  Chama Cha Mapinduzi CCm Mkoa wa Singida Juma Kilimba wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua na kupokea miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Manyoni na Itigi.

Kilimba amesema kwamba Serikali imejenga Madarasa mapya 632 kupitia fedha za miradi ya maendeleo kwa Mkoa huo hivyo kuwataka Madiwani na viongozi wa vijiji na kata kusaidia usimamizi wa matumizi ya majengo hayo na kuwataka kuhakikisha ukarabati unafanyika katika madarasa ya zamani ili yaweze kuendelea na matumizi.

“Haina maana kwamba kwa kuwa tumepata madarasa mapya mengine ya zamani tuyaache bila kuyakarabati, viongozi wa vijiji na kata kwa kushirikiana na madiwani kuona namna ya kukarabati majengo ambayo yanaonekana kuwa yamechoka ili yaendelee kutumika”. Alisema Kilimba

Akitolea mfano wa mijadala iliyoibuliwa katika kikao cha ushauri wa mkoa (RCC) kilichofanyika hivi karibuni mkoani hapo Juma Kilimba amesema  mkoa umetafiti mbinu mbalimbali za kuimarisha viwango vya ufaulu, mbinu za kutumia TEHAMA  katika kuondoa changamoto ya uhaba wa walimu hivyo majengo hayo yatakuwa na kazi kubwa  endapo yatakarabatiwa.

Akiendelea na ukaguzi wa miradi mbalimbali Mwenyekiti huyo akaishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya mama Samia Suluhu Hassani kwa kutoa kiasi kikubwa cha fedha ambapo katika kipindi cha mwaka 2022 wameweza kujenga miundombinu ya mabomba na kuchimba visima, ujenzi wa barabara za vijijini pamoja ujenzi wa vituo vya Afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa huo Dk. Binilith Mahenge akawataka ruwasa kuhakikisha wanajenga miundombinu ya maji iliyo imara ili kiuwasaidia wananchi kwa muda mrefu huku akiwakumbusha wataalamu hao kuhakikisha wanawasaidia wananchi waweze kuvuta maji majumbani mwao.

Aidha RC Mahenge akawataka wasimamizi wa miradi mbalimbali Mkoani hapo kuhakikisha kwamba fedha walizopewa zinatumika kama ilivyokubaliwa na kuleta tija kwa wananchi kwa kuwa lengo la serikali ni kuwanufaisha wananchi wake.

Wakiendelea na ukaguzi katika hospitali ya wilaya ya Manyoni Mwenyekiti wa halmashauri Jumanne Mlagaza pamoja na kuishukuru serikali kwa kuwapata fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo, akamuomba mwenyekiti kusaidia wazo la kupata eneo la kujenga hospitali kubwa ya wilaya kwa kuwa eneo walilonalo kwa sasa ni dogo na halina miundombinu mizuri ya barabara na majengo ya kutosha.

Hata hivyo Jumanne akaendelea kusema kwamba  miradi yote inayotekelezwa katika Halmashauri ya Manyoni inategemewa kukamilika kwa wakati pamoja na uwepo wa changamoto za mvua na baadhi ya vitu kupanda bei.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wa Wilaya ya Manyoni Melckzedek Humbe akitoa taarifa ya miradi yote wilayani hapo amesema halmashauri imepokea jumla ya Tsh. Bilioni 5.6 ambapo kati ya hizo Tsh.7.3 sawa na asilimia 75.9 ya fedha zilizotengwa.

Aidha Humbe  akasema kwamba miradi iliyotekelezwa  ni ukamilishaji wa vyumba vya maabara katika shule za sekondari, uchimbaji wa  visima katika maeneo mbalimbali na utekelezaji wa shughuli za TASAF.

Ziara hiyo inaendelea kesho katika wilaya ya Iramba na Ikungi baada ya leo kufanyika katika wilaya ya Manyoni na Halmashauri ya Itigi huku kikosi kingine kikendeleza na ziara hiyo wilaya ya Mkalama.

Ziara ikiendelea

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.