• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Kamati ya Siasa mkoani Singida yatembelea Miradi ya Ujenzi wa vyumba vya Madarasa

Posted on: January 19th, 2022

Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Singida leo Januari 19, 2022 imeanza ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia fedha za UVIKO 19 pamoja na fedha za tozo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM inayotekelezwa mpaka mwaka 2025.

Akiongoza ziara hiyo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida  Alhaji. Juma Kilimba  alisema lengo la ziara hiyo ni kukagua hali ya  utekelezaji wa Ilani ya chama kupitia fedha za UVIKO19  ambazo zimetumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa na vituo vya afya sehemu mbalimbali mkoani hapa.

Aidha, akiongea wakati wa ziara hiyo Alhaji Juma Kilimba  ameshukuru viongozi mbalikmbali wa Chama na  Serikali kwa usimamizi  madhubuti wa ujenzi wa vyumba hivyo na kuwakumbusha kwamba walipewa fedha hizo kwa kuwa waliamainiwa na Serikali ili kusimamia maendeleo kwa wananchi jambo ambalo amelitaka kuendelezwa.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo akatoa wito kwa wazazi na walezi  kuhakikisha watoto wanakwenda shule kwa kuwa tayari kila shule ina vyumba vya madarasa na madawati ya kutosha huku akiwataka walimu kuongeza juhudi ya kufundisha kwakuwa miundombinu ya elimu imeboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Akipongeza Serikali ya awamu ya sita, Alhaji Kilimba amebainisha kwamba imekuwa ikitekeleza kazi zake kwa uwazi zaidi na kwa kasi kubwa huku akitolea mfano wa ujenzi wa miradi ya vyumba vya madarasa  na vituo vya afya ambapo fedha za maendeleo zimekuwa zikija pamoja na maelekezo ya namna ya kuzitumia.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa  Singida Dkt. Binilith Mahenge  amesema Mkoa ulitengewa jumla ya Tsh. Bilioni 13.4 kwa ajili ya elimu msingi ikiwa ni fedha kutokana na mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa  na mapambano dhili ya UVIKO 19.

Aidha RC akaendelea kusema kwamba kiasi hicho cha fedha kilitakiwa kujenga jumla ya vyumba vya madarasa 662 ambapo 330 ni vyumba kwa ajili ya Sekondari na 332 kwa ajili ya Msingi  na vituo shikikizi.

Naye mjumbe wa kamati ya siasa ambeye pia ni Mkuu wa wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili amesema katika wilaya yake kulikuwa na miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Ntonge, Mandewa, Mrama, Ilongero, ujenzi wa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na nyumba ya mtumishi.

Miradi mingine ambayo inatekelezwa katika Manispaa ya Singida ni ujenzi wa  Barabara kwa kiwango cha Changarawe eneo la kindai, zahanati ya Unyianga na na kikundi cha utengenezaji wa thamani na kuchomelea madirisha alibainisha Mhandisi Muragili.

Aidha Mhandisi Muragili akaendelea kufafanua kwamba  ukiachilia mbali  fedha za UVIKO 19 zilizotumika katika ujenzi wa vyumba hivyo vya madarsa lakini kuna chumba kimoja cha darasa kilichopo katika shule ya Sekondari Mandewa ambacho kilinjengwa mpaka kukamilika kupitia fedha za tozo.

Akitoa taarifa yake Mkuu wa Wilaya  huyo alibainisha kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Singida Hospitali ya wilaya hiyo imepokea fedha kiasi cha  Tsh. Bilion 1.14 kwa ajili ya ujenzi wa wodi tatu ambazo ni chumba cha kuhifadhia maiti na nyumba kimoja kwa ajili ya  watumishi na  chumba cha wagonjwa mahututi ambapo ujenzi unaendelea.

Awali akitoa utambulisho kwa viongozi mbalimbali katika msafara huo, Katibu wa CCM Mkoa Singida  Lucy Shee alisema ziara hiyo inafanyika katika wilaya ya Manyoni na Itigi, Singida DC na Singida MC ambapo kesho ziara hiyo itaendela katika wilaya ya Ikungi, Iramba na Mkalama.

MATUKIO BAADHI KATIKA PICHA WAKATI WA ZIARA

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.