• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KASI YA UTEKELEZAJI YA MIRADI YA MAJI HALMASHAURI YA ITIGI INARIDHISHA.

Posted on: November 26th, 2017

  Utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Itigi umeonekana kuwa wenye kasi inayoridhisha licha ya halmashauri hiyo kuanzishwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Kaimu Kaibu Tawala Mkoa wa Singia Buhacha Baltazari Kichinda ametoa tathmini hiyo wakati wa kikao na wataalamu wa halmashauri hiyo ambapo wamejadili mikakati ya kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji.

Kichinda amesema ofisi ya Mkuu wa Mkoa haina wasiwasi kuhusu halmashauri kutekeleza na kusimamia miradi ya maji huku matarajio yakiwa ni ifikapo Juni 2018, asilimia ya upatikanaji wa maji ipande kutoka asilimia 34 za sasa hadi kufikia lengo la mkoa la asilimia 72.

“Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri mnaonyesha dhahiri mmejitosa kuwapunguzia wananchi adha ya kutafuta maji huku wakiacha kwa muda shughuli zao za uzalishaji mali, nina imani mtafikia asilimia 72 hata kabla ya Juni 2018 kwakuwa fedha mnazo na pia mnafanya usimamizi wa karibu wa miradi”, amesisitiza Kichinda.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Singida na hata halmashauri ya Itigi haina mito inayotiririsha maji mwaka mzima hivyo kusababisha uhaba wa upatikanaji wa maji katika kipindi cha kiangazi huku wananachi wakitegemea mabwawa na visima ambavyo vinatakiwa kujengwa na serikali.

“Kipidi cha Kiangazi kwakweli utawahurumia wananchi wanavyosumbuka kutafuta maji, wanatumia muda mwingi huko na kujikuta wana muda kidogo wa kuzalisha mali, hali hii haipendezi na nina imani pia viongozi wa Itigi hili haliwapendezi ndio maana mmeweka nia ya dhati kulitatua ili wananchi wapate muda mwingi wa kuzalisha kwaajili ya maendeleo ya Mkoa na taifa letu”, amefafanua Kichinda.

Naye Mhandisi wa Maji Mkoa wa Singida Lydia Joseph amesema endapo halmahauri hiyo itasimamia kwa umakini na haraka kukamilika kwa miradi ya Itigi mijini, Kitaraka na Aghondi itasaidia ongezeko la upatikanaji wa maji kwa asilimia 20.

Kwa upande wake Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya Itigi Evaristo Mgaya amesema halmashauri hiyo inatekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Rungwa, Ipande, Sanjaranda, Itigi, Kitaraka na Aghondi huku kukiwa na mradi wa visima 16 vya ‘windmill’ katika vijiji 12.

Mgaya ameeleza kuwa miradi hiyo itakamilika ndani ya kipindi cha mwaka huu wa fedha yaani kabla ya Juni 2018 hivyo kuongeza upatikanaji wa maji kwa zaidi ya asilimia 72.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi Luhende Pius Shija amesema wamewajibika sana kuboresha upatikanaji wa huduma za maji ambazo ni muhimu katika kukuza uchumi.

Luhende amesema licha ya kuendelea kutekeleza miradi iliyoko kwenye bajeti pia yeye na wataalamu wa idara ya maji wameongeza jitihada kwa  kuwasilisha maombi mengine ya kuonezewa fedha za miradi ya maji ambapo tayari wamekubaliwa hali itayaongeza zaidi upatikanaji wa maji.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.