• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KATIBU MKUU UTUMISHI ASISITIZA NIDHAMU KWA VIONGOZI NA WATUMISHI NCHINI.

Posted on: June 21st, 2017

  Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro amewataka viongozi na watumishi wote nchini kuzingatia nidhamu kama msingi wao wa utendaji kazi pamoja na kanuni na maadili ya utumishi wa umma ili utumishi wao uweze kuwa mzuri.

Dkt. Ndumbaro ameyasema hayo alipokutana na watumishi Mkoani Singida na kusikiliza matatizo, kero, changamoto pamoja na kupata maoni ya namna ya kuboresha utumishi wa umma kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma nchini.

Amesema kila mtumishi anapaswa kufanya kazi kwa bidii na kwa nidhamu ya hali huku akiwasisitiza viongozi hasa wa watumishi wa umma kuwasikiliza watumishi wao pale wanapotoa maoni yao bila kuyapuuzia au kuwakatisha tamaa kwa vitisho.

“Ukiwa kiongozi unapaswa uweze kuishi na kila aina ya mtu, kuna watumishi wengine hawawezi kufichaficha mambo ukikosea wanakusema bila kupepesa maneno, wengine ni waoga hawawezi kukueleza wazi ila wanatumia mbinu mbali mbali, ukiwa kama kiongozi uwe tayari kupokea ushauri ili uweze kuboresha utendaji wako”, amesisitiza Dkt Ndumbaro.

Dkt Ndumbaro amewaasa viongozi hao kuwapongeza watumishi wanaofanya kazi kwa bidii na wenye nidhamu ili iwe motisha kwa wale wavivu huku akiwataka kuwachukulia hatua wale wazembe na ambao hawataki kufuata kanuni na maadili ya utumishi wa umma.

“Unakuta mtumishi anajituma anafanya kazi kwa bidii, ana nidhamu na ni mbunifu lakini wewe kiongozi wake unamuangalia tu bila hata ya kumpongeza, hiyo inakatisha tamaa, inatakiwa umpongeze sio lazima umpe fedha hata barua tu ya kutambua utendaji wake itampa hamasa yeye na wenzake. Lakini pia kuna mwingine anakuwa hatekelezi wajibu wake unamtazama tu, hapo utawakatisha tamaa hata wale wachapakazi, amesema.

Aidha amewapongeza watumishi wenye vyeti halali huku akieleza kuwa zoezi la uhakiki wa watumishi bado ni endelevu ili kuhakikisha watumishi wanaobaki serikalini ni wale wanaostahili tu huku akiwashauri watumishi kuhakikisha wanasafisha taarifa zao muhimu ziwe halali na sahihi.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Mageni Lutambi amemshukuru Katibu Mkuu Utumishi kwa kuwatembelea watumishi wa Mkoa wa Singida na kusikiliza changamoto pamoja na maoni yao huku akiahidi kwa niaba ya watumishi kuwa wataendelea kuchapa kazi kwa bidi na nidhamu.

Dkt Lutambi amesema watumishi Mkoani Singida wanaadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma kwa kufanya kazi kwa bidi pamoja na kuongeza muda wa kufanya kazi kutoka saa tisa na nusu mchana mpaka saa kumi na nusu jioni ili kutoa muda zaidi wa kuwahudumia wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Linno Mwageni amemshukuru Katibu Mkuu Utumishi kuutembelea Mkoa wa Singida na kutoa maoni yake kuwa ili kuboresha utendaji hasa wa serikali za Mitaa inabidi serikali iwaajiri watendaji wa vijiji na kata wa kutosha.

Mwageni amesema watekelezaji wa shughuli na miradi ya serikali kwa ngazi ya mwananchi hasa ni watendaji wa vijiji na kata ambao kwa sasa ni wachache hivyo serikali iwaajiri wa kutosha ili waweze kufuatili kwa ukaribu miradi hiyo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.