• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AKEMEA VITENDO VYA RUSHWA.

Posted on: September 22nd, 2023

MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla.

Ametoa kauli hiyo tarehe 22 Septemba, mwaka 2023 muda mfupi baada ya kumaliza kutembelea, kukagua, kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru ambao umepokelewa kutokea Mkoani Tabora.

Akiwahutubia wananchi wa kata ya Kiomboi, Tarafa ya Kisiriri Wilaya ya Iramba Mkoani Singida muda mfupi baada ya kumaliza kukagua miradi ya maendeleo, amesema kuwa miradi mingi inakwama kutokana na watekelezaji au wasimamizi wa miradi hiyo kutoa au kupokea rushwa kwa nia ya kukinufaisha wenyewe.

Amesema kuwa ili kuwa na miradi bora na yenye kukubalika ni lazima kila Mtanzania kuhakikisha anapinga na kupiga kelele juu ya kuzuia vitendo viovu ambavyo vinatokana na vitendo viovu vya utoaji au upokeaji wa rushwa na kusababisha miradi au huduma kuwa chini ya ubora.

"Tunasema kuwa tupambane na rushwa kwa maana kwamba unaweza kuona kuwa mtu akitoa rushwa au kupokea rushwa anaweza kufanya kazi chini ya kiwango na kusababisha huduma kuwa mbovu.

"Tatizo la rushwa bado lipo nchini na imefika wakati watanzania wanaweza kuichukia Serikali yao kwa kukosa huduma nzuri pale mmoja anapokuwa amepokea rushwa au kutoa rushwa kwani ni wazi kuwa rushwa upotosha haki" amesema mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Akizungumzia suala la amani Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge kitaifa amewataka watanzania kuwa mabalozi waaminifu katika kutunza amani ya nchi kwa kusimamia amani, upendo mshikamano pamoja na kuendeleza na kulinda umoja wa kitaifa.

Kuhusu utunzaji wa mazingira Abdalla amewataka watanzania kuhakikisha wanatunza mazingira ili kuepuka kupata magonjwa yanayosababishwa na uchafu na kuepukana na kufanya shughuli za kibinadamu katika maeneo yenye vyanzo vya maji.

Amesema kwa sasa kuna hali ya mabadiliko ya tabia nchi hivyo ni vyema kuhakikisha watanzania wote kwa ushirikiano wa wanatunza vyanzo vya maji na kukaa zaidi ya mita 60 zaidi ya chanzo cha maji.

Sambamba na hilo Abdalla amesema ili kulinda nguvu kazi ya taifa ambapo asilimia kubwa ni vijana kila mmoja awe askari kwa lengo la kupambana na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Amesema kuwa vijana wengi ndo nguvukazi ya taifa hivyo wanatakiwa kutokutumia dawa za kulevya huku akiwashauri watanzaia kujiepusha na uagizaji, usambazaji pamoja na kilimo ambacho ni halamu.

Mwisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.