• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MADIWANI LIMENI ILI MUWE MFANO WA KUIGWA; RC NCHIMBi.

Posted on: September 14th, 2017

  Madiwani Mkoani Singida wametakiwa kulima mazao ya biashara kama vile Pamba na Korosho ambapo mazao hayo ni ya kipaumbele Mkoani hapa, ili kuonyesha faida za kilimo hicho kwa wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewaeleza hayo madiwani mapema leo katika mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat)-Mkoa, tawi la Singida uliofanyika katika ofisi za halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Dkt Nchimbi amesema madiwani wanapo hamasisha kilimo cha korosho na pamba kwa vitendo hasa kwa wao kuwa na mashamba yanayoonyesha zao hilo linastawi vizuri, wananchi wengi watahamasika na kujifunza kutoka kwao.

Ameongeza kuwa mkutano huo ulenge hasa katika kuangalia namna bora ya kumtumikia mwananchi na kuangalia njia mbalimbali za kumuokoa katika umaskini ili katika kuelekea Tanzania ya Uchumi wa kati na viwanda, asiwe mtazamaji bali mshiriki mkuu.

Dkt Nchimbi amesisitiza kuwa mkutano huo utumike pia kubainisha rasilimali zilizopo Mkoani Singida pamoja na fursa ambazo zinaweza kupatikana kutokana na uwepo wa rasilimali hizo.

“Singida tunazalisha ngozi na kuiuza ikiwa ghafi hivyo faida inakuwa ndogo, tumieni mkutano huu kuangalia uwezekano wa kuanzishwa kwa kiwanda kikubwa cha ngozi, ili tuanze sasa kuuza bidhaa za ngozi pamoja na kununua ngozi kutoka mikoa mingine nchini”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa ili kuboresha utendaji unaolenga kumsaidia mwananchi, maafisa utumishi wanapaswa kuwasimamia watumishi ili waweze kufanya kazi kwa bidii na uadilifu huku akiwataka wawapende watumishi wao.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat)-Mkoa, tawi la Singida James Mkwega amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa nasaha zake na kumuahidi kuwa mkutano huo utaweka malengo ya kuendeleza mkoa.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewaomba wananchi wa Singida kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu A. Lissu aliyejeruhiwa kwa risasi nyumbani kwake Dodoma.

Dkt Nchimbi amesema Lissu ni mwanasingida mwenzetu hivyo tunatakiwa kumuombea ili arejee katika afya yake na kuweza kuendelea na majukumu yake ya kuwatumikia wana Singida na Taifa kwa ujumla.

Aidha ameongeza kuwa hakuna anayefurahishwa kwa kitendo alichofanyiwa Lissu na kuwataka wanasingida na taifa kwa ujumla kuendelea kuliombea taifa liendelee kuwa kisiwa cha amani na utulivu.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.