• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Mfumo wa Kufundishia Masomo ya Sayansi Shule Za Sekondari Wafanyiwa Majaribio.

Posted on: February 25th, 2022

Mkoa wa Singida umejipanga kuboresha elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi na kuondoa daraja la mwisho (sifuri) katika shule za sekondari kwa kuanzisha mfumo wa kufundishia masomo ya sayansi kwa shule ambazo zina uhaba wa walimu wa masomo hayo. 

Akizungumza wakati wa majaribio ya kufundisha kwa kutumia mfumo huo wa kijiditali yaliyofanyika hivi karibuni katika Shule ya Sekondari Mitunduruni iliyopo Manispaa ya Singida, Katibu Tawala Mkoa huo Bi Dorothy Mwaluko amesema Mkoa umepanga kuongeza uelewa na ufaulu kwa wanafunzi wa Sekondari kwa kutumia video zilizohifadhiwa kwenye vifaa mbalimbali kama flash ili kufundishia mashule ambayo hayana walimu wa masomo hayo.

Katibu Tawala huyo amesema kufundisha kwa njia ya video kunamfanya mwanafunzi kuelewa kwa haraka kupitia njia tatu za ufahamu ambazo ni macho kuona, masikio kusikia na kuhisi kwa kugusa au kuandika na kuwataka walimu wa masomo hayo kujiandaa kutumia mfumo huo wakati marekebisho kadhaa ya kuuboresha yanafanyika.

Aidha Dorothy amebainisha kwamba jumla ya shule 142 za Serikali ndizo zitakazofaidika na mfumo huo  hasa zenye walimu wachache wa masomo ya sayansi kama hisabati phizikia na Kemia.

“Mfumo huo unatazamiwa kutumika mara tu mapendekezo ya maboresho ya mfumo yaliopendekezwa na walimu na wanafunzi wa shule hii na nyengine zitakazopata bahati yakufanyiwa majaribio”. Alisistiza Mwaluko.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Mitunduruni Mwalimu Victoria Calist akishukuru ujio wa programu na shule hiyo kuchaguliwa kuwa ya kwanza kufanyiwa majaribio hayo, amesema mfumo utawasaidia shule ambazo hazina walimu wa masomo husika na kukazia maarifa kwa shule ambazo tayari wanawalimu.

Amesema kwa mkoa wa Singida kuna upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya Sayansi yakiwemo hisabati na phizikia jambo ambalo lilikuwa likipunguza ufaulu wa wanafuzi hivyo uwepo wa mfumo huo utaondoa changamoto hiyo.

Aidha Mkuu wa Shule huyo akaomba   wataalamu wa TEHAMA kusaidia video kupatikana kwa njia ya  flashi au DVD ili wanafunzi waweze kujifunza wakiwa majumbani au mashuleni .

Hata hivyo Mwalimu Victoria alimshuku Afisa Tawala Mkoa pamoja na Mkuu wa Mkoa Dk. Binilith Mahenge kwa  ubunifu huo ambao utasaidia  kuondoa changamoto ya upungufu wa walimu wa sayansi mkoani Singida.

Silivanus Mputa ni mtaalamu wa TEHAMA ambaye alishirikiana na Afisa TEHAMA wa Mkoa Bw. Baraka Mhembano katika utengenezaji wa mfumo huo hapa anasema, utengenezaji wa mfumo huo wa kufundishia kwa kutumia video na sauti kwa sasa wamefanikiwa kutengeza vipinda vya masomo ya Hisabati Kiswahili na Baiolojia ambayo ndiyo yaliyotumika kufanyia majaribio.

Silivanus amefafanua kwamba vipindi hivyo vimegawanyika katika sehemu tatu (3) ikijumuisha  vilivyotengenezwa kwa kuonesha picha na sauti (real class) ambapo Mwalimu anafundisha kwa kuonekana, njia ya pili ni vilivyotengenezwa kwa njia ya wasilisho ambavyo vinakuwa na maandishi picha za mnato na sauti.

Njia nyingene ni video amabazo zimetengenezwa kwa njia ya uhuishaji (animation) ambazo zote zimetengenezwa na program mbalimbali ikiwemo adobe Premiere na Adobe photoshop. Alifafanua Silivanus.

Katika zoezi la kutumia mfumo wa kufundishia wanafunzi wa sekondari  umehusisha wanafunzi wa shule ya Mitunduruni iliyopo Manisiapaa ya Singida ambapo Aisha Haji Abdalah mwanafunzi wa kidato cha nne A akaishukuru Serikali ya mkoa ambayo imepanga kuboresha elimu.

Aisha ameeleza kwamba matumizi ya mfumo wa kufundishia masomo ya sayansi kwa shule za sekondari umeonesha wazi kwamba nchi ipo katika uchumi wa kati ambao unahitaji matumizi ya teknolojia katika kusambaza na kukuza maarifa kutoka mtu moja hadi mwingine.

https://www.blogger.com/blog/post/edit/6903235629886141782/128137890106155353

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.