• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MWAJIRI NA MWAJIRIWA SI MTU NA ADUI YAKE; DKT NCHIMBI.

Posted on: May 1st, 2017

   Waajiri wote Mkoani Singida hususani wakurugenzi wa halmashauri ambao ndio wenye watumishi wengi wameelekezwa kujenga mahusiano mazuri baina yao ili kuboresha utumishi wao.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi mkoani hapa yaliyofanyika katika uwanja wa Peolpe’s mjini Singida.

Dkt. Nchimbi amesema mwajiri na mtumishi sio maadui bali wanapaswa kujenga mahusiani mazuri hasa kwa mwajiri kujenga mazoea ya kufahamu sifa za watumishi wake, shida na matatizo yao.

Ameongeza kuwa waajiri wamekuwa wakisubiria watumishi wakosee ndio wawape adhabu lakini haipaswi kuwa hivyo kwani mwajiri anatakiwa ahakikishe anaweka mazingira mazuri na kumuelimisha mtumishi asifanye makosa.

“Ukiona mtumishi anafanya mambo yanayokinzana na sheria, kanuni na utaratibu, usimkaripie wala kumtega, mtafutie afisa ustawi wa jamii. Kwa vyo vyote afisa ustawi wa jamii atamrejesha kwenye mstari stahiki na mambo yatakwenda vizuri”.

Aidha Dkt Nchimbi amewataka wakurugenzi kutofanya ziara nyingi nje ya halmashauri zao bali wajikite katika kusikiliza na kutatua kero za wananchi na watumishi wao ambazo watazibaini endapo watafanya ziara za kutosha katika halmashauri zao.

Amesema ili kuboresha maslahi ya watumishi, waajiri wanapaswa kuandaa mafunzo kwa watumishi juu ya matumizi bora ya fedha ili waweze kutunza fedha zao, kila halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya watumishi kupewa viwanja vya makazi pamoja na kila halmashauri kuwa na afisa ustawi wa jamii atayehusika na watumishi kwa ajila ya masuala ya ushauri.

Pia Dkt. Nchimbi amekemea tabia mbaya ya baadhi ya wakuu wa idara/vitengo ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wafanyakazi wa kike walio chini yao.

“Wakuu hawa wa idara/vitengo wanakiuka sheria kanuni na taratibu kwa kuanzisha mahusiano ya kimapenzi humo humo kazini. Wakati mwingine wanafanya mapenzi na wake za watu. Tabia hii haikubaliki na haivumiliki hata kidogo. Viongozi au wakuu wa idara/vitengo wenye tabia ya aina hii, waiache mara moja”, amesema Dk.Nchimbi.

Kwa upande wao wananchi na watumishi Mkoani Singida wamempongeza rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua zake utumishi wa umma ambapo kwa sasa amerejesha nidhamu na uadilifu kwa kiwango cha kuridhisha.

Wananchi hao wamesema chini ya serikali ya awamu ya tano watumishi wa umma wamebadilika sana na sasa wanatoa huduma kwa ukarimu mkubwa, wepesi na uharaka zaidi tofauti na ilivyokuwa awali.

“Huko nyuma watumishi wa umma wengi walikuwa wana urasimu wa hali ya juu. Walikuwa wakitoa huduma huku macho na akili zao zikiwa kwenye ‘whatsapp’. Mbaya zaidi mwananchi ukipeleka kero zako, wanakuona ni msumbufu. Hivi sasa mambo ni tofauti kero za wananchi zinatafutiwa majibu na majawabu kwa wakati,” ameongeza Dkt. Nchimbi akiunga mkono maoni ya wananchi.

Mmoja wa wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo Sombi Hangida amekiri kwamba ni kweli watumishi wa umma wamebadilika mno na sasa wanatoa huduma bila kuomba rushwa na wamekuwa na lugha rafiki kwa wananchi.

Awali mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya wafanyakazi TUCTA Mkoani Singida Aaran Jumbe amehimiza kuhusu mabaraza ya wafanyakazi kufanyika katika maeneo ya kazi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu na hasa kuwashirikisha vyama vya wafanyakazi.

Jumbe ameongeza kuwa halmashauri zimekuwa zikitoa ushirikiano kwa vyama vya wafanyakazi na kuomba ushirikiano huo uendelee huku akisisitiza zawadi za mfanyakazi hodari zinazo ahidiwa na taasisi na halmashauri zitolewe kwa wakati.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.