• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MWENGE WA UHURU 2019 WAKABIDHIWA RASMI MKOANI TABORA

Posted on: August 26th, 2019

Serikali ya Mkoa wa Singida imekabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Tabora 26 Agosti, 2019 ambapo katika mkoa wa Singida Mwenge wa Uhuru umetembelea miradi 46 iliyohusu Sekta za Elimu, Afya, Mazingira, Maji, Utawala Bora, Kilimo, Ushirika, Biashara, na Programu za mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya, Malaria, Rushwa, Elimu ya Mpiga kura na UKIMWI. Miradi yote iliyokuwa inapitiwa na Mwenge wa Uhuru ilikuwa na thamani ya shilingi Bilioni 9,462,470,874.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, amesema miradi 12 ilikuwa inazinduliwa, miradi 2 ilikuwa inafanyiwa ufunguzi, miradi 10 ilikuwa inawekewa jiwe la msingi na miradi 22 ilikuwa inakaguliwa na kutembelewa.

Dkt. Nchimbi amesema, “Wananchi wa Mkoa wa Singida wameupokea vema ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 ambao umetolewa maeneo mbalimbali ya Wilaya za Mkoa wa Singida ambao ni: MAJI NI HAKI YA KILA MTU, TUTUNZE VYANZO VYAKE NA TUKUMBUKE KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA”.

Aidha, amesema, katika jitihada ya kuongeza huduma za Maji Mijini Mkoa wa Singida katika Miji ya Singida, Manyoni na Kiomboi imeingizwa kwenye Mradi Mkubwa wa Kitaifa utakaotekelezwa katika Miji 29 Tanzania kwa fedha za mkopo wenye masharti nafuu kutoka Serikali ya India.

Amesisitiza kuwa, katika Mkopo huo Miji ya Singida, Manyoni na Kiomboi imetengewa jumla ya shilingi 87 Bilioni. Hadi hivi sasa mtaalamu mshauri aliyeingia mkataba na Serikali kwa ajili ya kuandaa nyaraka za mradi huo anaendelea na kazi.

“Kipekee kwa niaba ya Uongozi wa Serikali, Wananchi, Marafiki na Wapenzi wote wa Mwenge wa Uhuru nikupongeze Ndugu Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru na Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa kazi kubwa na iliyotukuka ambayo mmeifanya kwenye Mkoa wa Singidda na Mikoa mbalimbali kwa Umakini, Umahiri, Weledi na Uzalendo mkubwa” amesema Dkt. Nchimbi.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa mkoa wa Singida amewashukuru na kuwapongeza Vijana wote Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kimkoa, Wilaya pamoja na timu zao, viongozi, Maaskari, Madereva na Wananchi wote kwa ujumla kwa kufanikisha kazi hii.

Kwa upande wake kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2019 Ndugu Mzee Mkongea Ali, amewashukuru Watendaji wote wa Mkoa wa Singida kwa ushirikiano wa dhati walioupata wakati wote walipokuwa katika Wilaya za Mkoa wa Singida.

Pia amewapongeza kwa miradi mizuri ya maendeleo tumeona kwa namna gani mnavyopaambana na adui ujinga tumeona viwango vizuri vya shule, tumeona kwa namna gani ambavyo mnapambana na adui maladhi tumeona vituo vya afya vyenye viwango ya hali ya juu, tumeona kwa namna gani mnavyopambana na adui maskini tumeona kwa namna gani asilimia 10 inavyomfikia mlengwa" Amesema Ndugu Mzee Ali Mkongea.

Akihutubia kwa nafasi mbalimbali, Ndugu Mzee Mkongea, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kwenda kupiga kura kwa amani na usalama, kujitokeza kwenye mikutano ya kampeni ili kwenda kusikiliza sera, ili kuweza kumpima kiongozi kama anafaa au hafai.

"Hivyo nichukue fulsa hii, kuwasihi kwenda kuchagua viongozi bora waadilifu, waaminifu ambao wana kariba kama ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli." Amesema Mkongea.


Imetolewa na;

Kitengo cha Habari na Mawasiliano

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

SINGIDA

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.