• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

NMB IWASAIDIE WAFANYABIASHARA SINGIDA KUANZISHA KIWANDA CHA VIFUNGASHIO; DKT NCHIMBI.

Posted on: September 18th, 2017

  Benki ya NMB imetakiwa kuwasaidia wafanyabiashara Mkoani Singida kuanzisha kiwanda cha kutengenea vifungashio, ili waweze kuhifadhi bidhaa zao katika ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo mapema leo wakati akifungua warsha ya siku moja ya klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB, katika ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.

Dkt Nchimbi amesema klabu hiyo ya wafanyabiashara itaweka alama kubwa katika maendeleo endapo watajipanga na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza vifungashio hivyo kuliko kuendelea kuvifuata nje ya Singida au nje ya nchi.

“Uzoefu usipotumika vizuri unaweza ukawa kikwazo cha kuendelea, msizoee kufuata vifungashio na label nje ya singida wakati fursa ipo ya kuanzisha kiwanda hicho Singida”, amesema na kuongeza kuwa,

“Wafayabiashara mzipende biashara zenu na kuziweka katika hali ya usafi na yenye kuvutia, wengine wanapenda kujisafisha na kujipendezesha wenyewe lakini ukiangalia biashara zao hazivutii, zimewekwa tu bila kufungashwa vizuri”, amesisitiza.

Aidha amewataka wafanyabiashara wasiogope kukopa kwakuwa sio jambo la aibu wala fedheha, ila kinachotakiwa ni kuwa na nidhamu ya mkopo na malengo ili waweze kufanikiwa.

“Akina mama jifunzeni kuwa na nidhamu ya mkopo, sio unakopa leo mara unasikia kapu la mama, jifikirie hayo ndio malengo ya huo mkopo hata kama ni jambo muhimu?, nidhamu ya mkopo inatakiwa ianze kabla ya kukopa na iendelee kuwepo.

Dkt Nchimbi pia ameishukuru benki hiyo kwa kushirikiana na serikali katika mambo mbalimbali ya kielimu na afya, pia amewashukuru kwa kutoa mikopo kwa watumishi wa umma jambo ambalo linawasiadia katika mambo mbalimbali.

Naye Meneja wa NMB Kanda ya kati Straton Chilongola amesema klabu za wafanyabiashara nchini ziko 34 ambazo zimekuwa zikipatiwa mafunzo mikopo kutoka katika benki hiyo.

Chilongoloa amesema benki hiyo imekuwa ikitoa mafunzo juu ya ulipaji kodi, ujasiriamali, masuala ya mitaji, leseni na ardhi ili wafanyabiashara hao waweze kukuza mitaji yao.

Amesema benki hiyo imefanikiwa kuwakuza wafanyabiashara wengi ambazo wameanza nao wakiwa wafanyabiashara wadogo ambapo sasa wamekuwa wakubwa na wakati huku wakiajiri wengine na hivyo kukuza uchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB Singida Emmanuel Rweyemamu Kyoma amesema wazo la kuanzisha kiwanda cha kutengeza vifungashio wamelipokea vizuri huku wakijipanga kuandaa andiko kwa ajili ya kiwanda hicho.

Kyoma amesema kwa ushirikiano na NMB kiwanda hichokitaweza kujengwa Singida huku wakimuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa Mkoa wa Singida utazalisha chakula cha kutosha kulisha Mkoa wa Dodoma.

Amesema benki ya NMB imekuwa ikishirikiana na wafanyabiashara hao hivyo mipango ya kukuza uchumi kama huo wa kuanzisha viwanda utatekelezeka bila matatizo yoyote.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.