• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) YATOA MAFUNZO YA MPANGO WA SHULE SALAMA KWA WASHIRIKI KUTOKA MIKOA MINNE*

Posted on: August 12th, 2024

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) leo imeendesha mafunzo maalum ya Mpango wa Shule Salama, yaliyowakutanisha washiriki 275 kutoka mikoa ya Singida, Shinyanga, Tabora, na Simiyu. Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika mkoani Singida, yakilenga kuwajengea uwezo washiriki ili kuhakikisha shule za sekondari zinatoa elimu bora kwa kuondoa vikwazo mbalimbali vinavyowakabili wanafunzi.

Mafunzo haya yamehusisha wenyeviti wa bodi za shule za sekondari 150, maafisa 12 kutoka ngazi za mikoa, maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya mkoa, pamoja na waratibu wa Mpango wa Shule Salama. Aidha, waratibu wa programu ya SEQUIP pia walishiriki katika mafunzo haya, ambayo ni sehemu ya Mpango wa Kuboresha Elimu ya Sekondari wa miaka mitano (2020-2025).

Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwapatia stadi na mbinu za usimamizi bora wa shule za sekondari ili kuhakikisha elimu inayotolewa inakidhi viwango vilivyokusudiwa. Mafunzo haya yanazingatia kuondoa vikwazo kama vile ukosefu wa chakula, utoro, na matumizi ya viboko, ambavyo mara nyingi huzuia wanafunzi kufikia malengo yao ya ufaulu. 

Mafunzo haya yanatarajiwa kuwawezesha washiriki kuleta mabadiliko chanya katika shule zao, na hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi wa sekondari nchini.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Elipidus Baganda, akizungumza kwenye mkutano na washiriki wa programu ya Shule Salama amesisitiza umuhimu wa elimu bora kwa wanafunzi kama msingi wa maendeleo ya taifa.

Aidha, alieleza jinsi Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inavyoendelea kutambua na kuthamini elimu kama chombo muhimu cha kuleta maendeleo.

Dkt. Baganda alibainisha kuwa kumekuwepo na changamoto ya mdondoko wa wanafunzi katika shule za msingi na sekondari, jambo linalozuia wanafunzi kufikia malengo ya kielimu ambapo amesema Serikali imechukua hatua mbalimbali kupambana na changamoto hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa elimu bila malipo na kujenga shule za sekondari karibu na makazi ya jamii, ili kupunguza umbali wa kufuata shule.

Alieleza kuwa Serikali imeanzisha Mpango wa Shule Salama katika shule za sekondari nchini kwa lengo la kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji, pamoja na kuongeza ulinzi na usalama wa watoto.

Hata hivyo, Dkt. Baganda amewashukuru wadau wote wanaoshiriki katika kusimamia utekelezaji wa mpango huo na kuwataka washiriki wa mkutano huo kujadiliana na kubadilishana uzoefu ili kuboresha utekelezaji wa mpango wa Shule Salama na kuwataka washiriki kutumia mafunzo hayo kuibua mbinu mpya za kuboresha mazingira ya shule na kuhakikisha wanafunzi wanakamilisha mzunguko wa elimu kwa mafanikio.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.