• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Ofisi za Shule Bora zafunguliwa rasmi Mkoani Singida.

Posted on: November 28th, 2022

Mkoa wa Singida umesema mikakati mbalimbali ya kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa elimu katika shule za Sekondari na Msingi kama sehemu ya ushirikiano na wadau wengine wakiwemo shule bora katika kuimarisha elimu kwa watoto wote.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Stanslaus Choaji, wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Mradi wa shule bora Mkoa wa Singida ambapo alieleza juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau hao kuboresha ujifunzaji, ufundishaji na ujumuishi wa elimu ya Msingi na Sekondari.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Stanslaus Choaji, akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Aidha Choaji ameeleza kwamba kwa kutoa eneo la ujenzi wa Ofisi kwa ajili ya mradi huo inadhihirisha uhusiano mzuri uliopo baina ya Serikali ya Mkoa na mradi wa shule bora jambo ambalo ameeleza kwamba linaweza kuleta matunda na kufikiwa kwa malengo ya Serikali na mradi huo.

Hata hivyo Kaimu Katibu Tawala huyo ametoa pongezi kwa timu ya Mradi wa Shule bora kwa namna ambavyo wameanza kutekeleza majukumu yao mbalimbali kupitia Halmashauri za Mkoa huo.

Choaji ameahidi kwa Niaba ya Serikali ya Mkoa kushirikiana na wadau hao kufanikisha mipango waliojiwekea kumkomboa mtoto wa shule ndani ya Singida na Taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Kitengo cha huduma ya Jamii Ubalozi wa Uingereza Getrude Mapunda, akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha huduma ya Jamii Ubalozi wa Uingereza Getrude Mapunda, amesema Mradi hauanzishi vitu vipya zaidi unatekeleza mipango ya Halmashauri ili kuunganisha rasilimali fedha na rasilimali Watu kutoka Serikali na mwenye Mradi ili kuwasaidia watoto wa kitanzania.

"Mradi hauna fedha nyingi kuliko za Serikali hivyo tukichanganya fedha nyingi za Serikali na zile kidogo za Mradi tunaweza kufikia malengo ya Halmashauri zilizojiwekea katika kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondari " alisema Getrude.

Hata hivyo ameomba ushirikiano uliopo uendelee baina ya Mkoa wa Singida na shule bora ili kufikia malengo waliyojiwekea huku akibainisha kwamba changamoto za wanafunzi mashuleni zinatofautiana kwa kila Mkoa.

Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoani Singida Samweli Daniel, akitoa taarifa wakati wa hafla ya uzinduzi huo.

Awali akitoa taarifa yake kwenye Mkutano huo Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoani Singida Samweli Daniel, amewapongeza viongozi wa Shule bora ambao wametokea Ubalozi wa Uingereza kuja kwenye uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Amesema uwepo wa Ofisi hizo utasidia sana katika utekelezaji wa majukumu yao hasa kuhakikisha shule bora inaboresha ujifunzaji, ufundishaji, ujumuishaji na uimarishaji wa mifumo ya elimu.

Amesema kupitia Mradi huo watahakikisha changamoto hizo zinazokabili elimu mkoani hapo zinakwisha na watoto wanapata elimu Bora kwa usawa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.