• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAIS SAMIA ATIMIZA AHADI KUCHANGIA MSIKITI,RC DENDEGO ASHUHUDIA.

Posted on: January 10th, 2025

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametekeleza ahadi yake ya kutoa Sh.Milioni 50 kwa  ajili ya ujenzi wa msikiti wa Taqwa ambayo aliitoa kupitia kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Ally Hapi.

Katibu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida, Omari Muna, alikabidhi hundi ya malipo ya fedha hizo jana kwa Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro hafla iliyoshudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Halima Dendego na waumini, iliyofanyika Januari 10,2025.

Hapi akizungumza kwa njia ya simu alisema Rais amekuwa akisaidia mara kwa mara ujenzi wa misikiti na makanisa kutokana na mapenzi makubwa aliyonayo kwa Watanzania hivyo wananchi warudishe shukrani kwake kwa kuendelea kumuombea.

Alisema fedha hizo zitumike vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa ili rais na  wadau wengine wanapoona kazi imefanyika vizuri waone umuhimu wa kuendelea kutoa zaidi kwa ajili ya ujenzi wa msikiti huo.

" Niwaombe tuendelee kumuombea dua na afya njema Rais wetu kwani mambo anayoyafanya ni kutokana na mapenzi makubwa aliyokuwa nayo kwa Watanzania na ninampongeza Sheikh wa mkoa kwa kuwashirikisha waumini katika suala hili la ujenzi wa msikiti,” alisema.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Singida, Nassoro, alimshukru Rais Dk.Samia kwa mchango wake huo na kuwataka wananchi kuendelea kumuunga mkono rais kutokana na mambo makubwa ya maendeleo anayoyafanya katika nchi yetu.

Sheikh Nassoro alisema katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025 wananchi waendelea kudumisha amani na upendo kama ilivyoasisiwa na waasisi wa Taifa hili.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Halima Dendego, alimshukuru Mhe. Rais Dk. Samia kwa mchango huo wa ujenzi wa msikiti ambapo aliunga mkono kwa kuchangia Shilingi Milioni 5.

“Tunawashukuru wale wote walioguswa katika kuchangia ujenzi wa Msikiti huu ambapo zimefikia jumla Shilingi milioni 176 , kila mmoja aliyeguswa apate baraka za Mungu,” alisema Mhe.Dendego

Hata hivyo, alisema malengo ya ujenzi huu bado hayajafikiwa hivyo Waislam na wadau wengine waendelee kuunga mkono kwa kuchangia pesa hasa ikizingatia msikiti huo upo katikati ya mji wa Singida, hivyo ni lazima uonekane wa kisasa.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.