• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC DENDEGO AWAAHIDI NEEMA WALIMU, AHIMIZA KUENDELEA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KUONGEZA UFAULU NCHINI

Posted on: May 16th, 2024

Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanatatua changamoto na matatizo mbalimbali yanayowakabili Walimu katika maeneo yao ili kuongeza ari katika ufundishaji na ufaulu wa wanafunzi mashuleni.

Dendego, ametoa maagizo hayo (tarehe 16 Mei, 2024) katika ufunguzi wa Kongamano la Siku Mbili la Walimu kutoka mikoa ya Kanda ya kati na Kaskazini ambao wamekutana mjini Singida kujadili masuala mbalimbali yanayoikabili sekta hiyo ikiwemo namna bora ya kutetea maslahi yao na kuweka mipango na mikakati madhubuti ya kuongeza maradufu ufundishaji na ufaulu katika maeneo yao ya kazi.

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa amesisitiza kuwa matatizo mengi yanayowakabili Walimu yanaweza kutatuliwa na Viongozi waliopo ngazi za Wilaya kwa kukaa pamoja na kujadili kwa kina namna bora ya kutafuta majawabu sahihi ambayo yataongeza ari ya Walimu kufundisha na kupandisha ufaulu kwa wanafunzi.

Amesema Serikali ya awamu ya Sita imefanya mambo makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Elimu hivyo ni muhimu kwa Walimu kote nchini kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu mkubwa ili kutengeneza Wanafunzi bora ambao watalisaidia Taifa kusonge mbele Kimaendeleo haraka.

Kuhusu maadili ya Wanafunzi, Mheshimiwa Halima Dendego, amewahimiza Walimu kuhakikisha wanawalea wanafunzi katika njia sahihi kwa kuzingatia mila na desturi za kitanzania ili kuwaepusha na matatizo ya utovu wa nidhamu.

Hata hivyo, Dendego, amewataka Walimu kutoa adhabu stahiki kwa wanafunzi wanaoenda kinyume na taratibu za shule kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo nchini ili kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza shule au vyuo wanakuwa na maadili mazuri yanayompendeza Mwenyezi Mungu, Jamii na Taifa kwa ujumla.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, amewataka Walimu kuzingatia kanuni na taratibu katika malezi ya wanafunzi ili kukabiliana na tatizo la mimba kwa wanafunzi jambo ambalo amesema halipendezi hata kidogo.

Dkt. Fatuma Mganga, amewahimiza Walimu kuongeza bidii na ubunifu katika ufundishaji ili kuhakikisha Taifa la Tanzania linapata Watalaamu wazuri na wabobezi ambao watasaidia nchi kusonga mbele kimaendeleo haraka.

Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania -CWT- Leah Ulaya, ameiomba Serikali kuendelea kushughulikia matatizo yanayowakabili Walimu ikiwemo ulipaji wa madeni na upandishaji wa vyeo kwa wakati jambo ambalo amesema litasaidia Walimu kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Rais huyo pia amewahakikishia Viongozi wa mkoa wa Singida na Taifa kwa ujumla kuwa wataendelea kufanya kazi kwa bidii kwa sababu wanaimani na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na mwanamama shupavu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, inafahamu kilio chao na itaendelea kutatua changamoto zinazowakabili kwa haraka.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.