• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Mahenge Awaasa Wakurugenzi na DC Kukamilisha Miradi ya Ujenzi Wa Vyumba vya Madarasa Kwa Wakati.

Posted on: November 1st, 2021

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Bi Doroth Mwaluko wakati akitoa miongozo mbalmbali katika kikako kilichofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa ambacho kilichowakutanisha Wakuu wa wilaya na Wakurungezi wa Halmashuri zote za Mkoa wa singida.

Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya  Mkoani Singida wametakiwa kukamilisha jumla ya vyumba vya madarasa   662 na mabweni mawili (2) kabla ya kufikia  katikati ya mwenzi Decemba 2021 ambavyo vinahitajika kwa ajili ya kidato cha kwanza  mwaka 2022.

Hayo yamebinishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge leo 01.11.2021 katika ukumbi wa mikutano ofsini hapo ambapo aliwakutanisha wakuu wa wilaya pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Singida .

Amesema Serikali imetoa fedha za maendeleo kiasi cha shilingi bilioni 6.6 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 330 ambavyo vinahitajika  kwa ajili ya kidato cha kwanza mwaka 2022 na vyumba  332 vya madarasa  vitakavyo gharimu jumla ya shilingi bilioni 6.6 kwa ajili ya ujenzi wa vituo shikizi vya shule za msingi .

Hata hivyo Mkuu wa mkoa amebainisha kwamba katika fedha za maendeleo zilizokuja jumla shilingi milioni 160 zitatumika kujenga mabweni mawili (2) katika shule za msingi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Amesema katika kutekeleza mpango wa maendeleo kwa usatwi wa taifa na mapambano dhidi ya uviko 19, Mkoa umetengewa fedha zaidi ya shilingi   Bilioni 27.068 kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika sekta ya Afya, elimu na maji.

Hata hivyo Dkt. Mahenge amewataka Wakurugezi wa Halmashauri ya Itigi na Mkalama kuhakikisha wanafuatilia kwa ukaribu fedha ambazo zilikuwa bado hazijaingia katika baadhi ya mashule ziweze kuingia na kufanyiwa kazi iliyokusudiwa.

Dkt. Mahenge amewakumbusha viongozi wote wa Hamashauri za wilaya kutosafiri kipindi hiki cha utekelezaji wa miradi hiyo ili kuimarisha usimamizi kama muongozo wa awali ulivyotolewa aliendelea kusema Mkuu wa Mkoa huo.

Akimalizia maagizo yake Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashuri hizo kufanya manunuzi ya pamoja (bulk procurement) ili kupunguza gharama za utekelezaji wa miradi hiyo na kuwahimiza Mameya  wenyeviti wa Halmashuri,  watendaji wa Halmashauri na madiwani kusimamia miradi hiyo Kikamilifu.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida Bi Doroth Mwaluko  akawakumbusha Wakurugenzi hao  kutekeleza maagizo   yaliyotolewa na Ofis ya Rais  Tamisemi juu ya maandalizi ya utekelezaji wa mpango kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya uviko 19.

 Bi. Doroth akatumia muda huo kuagiza  kuundwa kwa timu maalum za mkoa na Halmashauri  ambazo zitakuwa zikifuatilia miradi  hiyo ya maendeleo ya Afya, Elimu na Maji  kama maagizo yalivyotolewa na Wizara ya  Tamisemi.

Aidha akawakumbusha kuhakikisha miradi yote inayokamilika pamoja na ununuzi wa vifaa unawekwa alama  ya mpango wa maendeleo kwa ustawi na mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO -19 ili kuzitambua na kuweza kutofautisha.

Tovuti za Halmashauri pamoja na Mkoa zitumike kikamilifu kutangaza kazi za utoaji wa huduma kwa wanunuzi wa Vifaa na mafundi ili atakayeweza kutoa huduma stahiki apate fursa hiyo, alikaririwa Bi Doroth Mwaluko.

Awali  katika wasilisho lake Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Mipango na uratibu  Bi Beatrice Mwinuka akabainisha kwamba katika jumla ya fedha zote zilizokuja wametanga shilingi bilioni 13.4 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Elimu msingi ambayo ndiyo itakayotumika katika ujenzi wa vyumba 632 na mabweni mawili (2) .

Aidha akaendelea kufafanua kwamba jumla ya shilingi bilioni 9.6 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu  na ufuatiliaji wa Afya ya msingi ambapo kutakuwa na ujenzi na ununuzi wa vifaa vya  huduma ya dharula (EMD),ujenzi wa majengo ya wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na unuuzi wa X-rays

Beatrice akaendelea kueleza kwamba fedha hizo zimetengwa kwa ajilia ya uboreshaji wa miradi tisa (9) ya maji  itakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.04 katika wilaya ya Iramba , Mkalama, Singida  Ikungi, Manispaa ya Singida pamoja na wilaya ya  Manyoni.

 MWISHO  

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.