• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Mahenge awataka Viongozi Mkoani Singida kutatua Kero za wananchi

Posted on: July 5th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na watendaji katika wilaya zote za mkoa huu kufanya ziara kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi badala ya kusubiri viongozi wa Serikali ya mkoa ndio wazitatue changamoto za wananchi.

Ametoa agizo hilo wakati wa kikao maalum cha kufanya majumuisho ya ziara yake aliyoifanya hivi karibuni katika wilaya zote za mkoa huu kwa ajili ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.

Dk.Mahenge alisema serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo lakini wananchi hawajui kinachoendelea kwasababu viongozi ambao wanapaswa kuwaeleza hawafanyi hivyo.

"Ni muhimu mno kufanya mikutano ya wananchi kusikiliza kero zao, wahamasisheni madiwani, makatibu tarafa wafanye ziara, mkoa wetu mwaka wa fedha uliopita tulipata Sh.230 bilioni ni wajibu wetu kama viongozi kuzisimamia ili zilete tija katika maendeleo," alisema.

Dk.Mahenge alisema wakuu wa wilaya wanajitahidi sana kufanya ziara na kusikiliza kero za wananchi lakini changamoto ipo kwa watendaji wengine wa serikali ambao hawafanyi hivyo na hivyo kusababisha kuibuka kwa kero nyingi ambazo kama ziara zingekuwa zinafanyika hali hiyo isingejitokeza.

Aliongeza kuwa katika baadhi ya maeneo wananchi wamekuwa wakilalamika kutoshirikishwa kwenye mipango mbalimbali ya maendeleo hususani baadhi ya wenyeviti wa serikali za vijiji ambao ndio wamekuwa na tabia hiyo.

"Baadhi ya wenyeviti wa vijiji wamekuwa kama miungu watu hawatowi fursa ya kusikiliza wananchi, RAS (Katibu Tawala Mkoa) tufanye uchunguzi na tuchukue hatua kwa kuzingatia sheria na taratibu za serikali," alisema Dk.Mahenge.

Aidha, Dk.Mahenge aliagiza wakuu wa wilaya kwa kushirikiana na wataalam wa ardhi kufuatilia migogoro yote ya ardhi na kuipatia ufumbuzi na kuiweka kwenye 'data base'.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa huo kuwa yote aliyoyaagiza atayafanyia kazi kwa kushirikiana na Watendaji wa Halmashauri za Mkoa.

MWISHO

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.