• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC NCHIMBI AAGIZA MIZINGA 50 YA NYUKI KWA TIMU YA STAND MISUNA, AIPONGEZA KWA KUREKEBISHA TABIA.

Posted on: May 26th, 2017

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi ameiagiza halmashauri ya Manispaa ya Singida kusimamia upatikanaji wa mizinga hamsini ya nyuki kwa ajili ya timu ya mpira wa Miguu ya Misuna Stand kwakuwa imekua ni timu yenye lengo la kuwa kituo cha mafunzo na marekebisho ya tabia.

Dokta Nchimbi ametoa agizo hilo mapema leo asubuhi alipokutana na wananchama wa klabu hiyo ambapo amewaomba radhi kwakuwa Mkoa, wilaya na Halmashauri ya manispaa imekuwa haitoi ushirikiano wa kutosha kwa timu hiyo.

Amesema timu hiyo ambayo imeundwa na umoja wa Mawakala wa Mabasi Singida, imekuwa mstari wa mbele wa kubadilisha tabia mbaya kuwa njema hasa kutokana na mazingira ya stendi nyingi nchini kutawaliwa na vitendo vya uvunjaji wa sheria.

Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa sasa serikali ya Mkoa, wilaya na halmashauri imewatambua na kwa kuthibisha hilo yeye kama mkuu wa mkoa amejiunga ramsi kama mwananchama wa timu hiyo ya mpira wa miguu na kutoa michango ya miezi mitatu ambapo kila siku mwanachama anatakiwa kuchangia shilingi miatano.

“Nimetoa ada ya uanachama kuonyesha kuwa tupo pamoja na tutashirikiana kuhakikisha timu yetu ya Misuna Stand inapanda daraja, kwa sasa nawaomba wanachama wote tushirikiane katika kuiboresha timu yetu”, amesisitiza.

Dkt. Nchimbi amesema lengo la Mkoa ni kuwa na timu mbili za mpira wa miguu ambazo zinashiriki ligi kuu na kwakuwa tayari uwanja wa nyumbani wa Namfua Stadium uko katika hatua za mwisho za ukamilishaji huku akiwahakikishia mashabiki wa Singida United kuwa wataishuhudia timu yao ikicheza nyumbani.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo ambaye ameteuliwa kuwa Mlezi wa Timu hiyo amesema stendi zimekuwa ni mahala pa wizi, uvutaji wa madawa ya kulevya na vitendo viovu lakini jitihada za Misuna Stand FC zitabadilisha tabia hizo na kuwa njema.

Tarimo amesema wanachama watakuwa wachapakazi kwakuwa kila siku wanatakiwa kulipa kiasi cha shilingi miatano lakini pia wamejipanga kuhakikisha wanaelimishana juu ya madawa ya kulevya jambo ambalo litaufanya Mkoa na Mji wa Singida kuwa wa Amani sana.

Ameongeza kuwa atahakikisha anasimamia utekelezaji waq agizo la Mkuu wa Mkoa La kuipatia timu hiyo Mizinga hamsini pamoja na kuhakikisha halmashauri inatoa eneo la utundikaji wa miznga hiyo pamoja na kuitunza.

Naye Mwenyekiti wa tawi la Misuna stand FC Yahya Said Kisiu amesema wanachama wa timu hiyo wamepata faraja kubwa sana kwa kutembelewa na Mkuu wa Mkoa pamoja na kuwapatia mizinga hamsini.

Kisiu ameongeza kuwa timu hiyo iliyoanzishwa mwaka 2014 ilifanikiwa kufika ligi daraja la pili lakini kwa sasa imeshuka tena daraja huku akisisitiza kuwa ari mpya waliopatiwa mkuu wa Mkoa itawezesha timu hiyo kupanda tena daraja.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.