• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba amaliza Mgogoro wa mashamba ya Mpambaa na Kinampundu Mkoani Singida uliodumu kwa miaka zaidi ya miwili.

Posted on: September 28th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba leo tarahe 28.09.2022 amemaliza mgogoro wa shamba la mbegu lililopo Kata ya Mpambaa Wilaya ya Singida Vijijini na Kinampundu Wilaya ya Mkalama lenye  ukubwa wa ekari 456.82 uliodumu kwa miaka zaidi ya miwili.

Akiongea katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa kata hizo mbili Mkuu wa Mkoa amesema shamba hilo litagawanywa katika sehemu mbili ambazo ni  ekari 222.5 zitakazo milikiwa na  Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama na ekari 234.32 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Vijijini kwa kuzingatia mipaka iliyoainishwa kisheria kwenye G.N.

“Timu ya Wataalam iliyoundwa ilipitia mipaka ya kisheria kwa mujibu wa G.N. Na. 160 ya tarehe 15 Novemba, 1935, GN Na. 287 ya 9 Septemba, 2011 zinazohusu Halmashauri ya Wilaya ya Singida na Tangazo la uanzishaji Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama la 26 Juni, 2013”. Alisema

Aidha, Rc Serukamba amesema kwamba Halmashauri zote mbili ziyapime mashamba hayo yaliyogawanywa na kuyasimamia uendeshaji wake ili wananchi wa Vijiji husika wanufaike kwa kuendeleza kilimo, ufugaji na shughuli nyinginezo za uzalishaji mali.

Rc Serukamba akabainisha kwamba Vijiji vilivyopo eneo la mashamba hayo vipewe kipaumbele cha kuandaliwa mipango ya matumizi Bora ya ardhi ili kuepuka migogoro mingine ndani ya maeneo ya Utawala wa Vijiji.

Hata hivyo Serukamba akaagiza kuwekwa alama za mipaka (Beacon) maeneo ya mita 100 mpaka 200 kwenye maeneo ya mpaka na wananchi wapewe elimu ili kuepuka migogoro kama hiyo kutokea tena.

Mkuu wa Mkoa huo ameziagiza Halmashauri hizo pamoja na Serikali za Vijiji katika mashamba hayo zihakikishe wananchi watakaopewa maeneo ya mashamba hayo wahakikishe wanayalima ili yasiwe Mashamba pori huku akisistiza mgao huo uwalenge zaidi vijana na wanawake ili kupunguza tatizo la ajira.

Awali Mkuu wa Mkoa alisema kwamba Shamba la mbegu la Mpambaa lililokuwa linamilikiwa na Mkoa wa Singida, ambalo limekuwa likutumika kwa shughuli za Kilimo. Aidha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ilipokea malalamiko kuhusu umiliki halali wa shamba hilo mwezi Februari, 2022 kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida au Mkalama.

Katika kutatua, sintofahamu hiyo, Mkoa uliunda timu ya Wataalam iliyopewa hadidu za rejea zilizojumuisha kubaini eneo la shamba, kubaini liko katika mamlaka ya Halmashauri gani na uendeshaji wake.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.