• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba, amewataka Makarani na Wasimamizi wa SENSA mkoani hapa kutanguliza uzalendo katika zoezi la SENSA

Posted on: August 16th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amewataka Makarani na Wasimamizi wa SENSA mkoani hapa wasifanye zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kama ni la kuja kutafuta posho tu.

Akizungumza na Makarani na Wasimamizi hao ambao wanaendelea na mafunzo mjini Singida, alisema jukumu walilopewa ni kubwa sana linahitajika kufanywa kwa umakini ili taifa lipate takwimu sahihi za watu kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo.

"Zoezi hili ni kubwa la kitaifa ambalo linahitaji umakini wa hali ya juu na watakalofanya lifanikiwe ni nyie hivyo tusilifanye zoezi la Sensa kama ni la kuja kutafuta posho, inawezekana wengine wapo hapa na vishikwambi anayofundishwa haelewi kikubwa muhimu kwake apate hela jioni, utakuwa hujaisaidia nchi yako," alisema.

Serukamba alisema kupitia Sensa hii nchi itaweza kujua idadi ya maskini, watu wanahitaji shule, afya  na maji kiasi gani hivyo vijana watambue wameaminiwa na nchi waifanye kazi ya Sensa kwa umakini sana.

Alisema mtihani kwa wasimamizi na makarani wa Sensa ni kuifanya kazi kwa weledi na kuleta takwimu sahihi ambapo wakiifanya vizuri kazi hii Serikali itakapokuwa na kazi nyingine wao ndo watapewa kipaumbele  kupewa.

"Mkoa unawategemea sana kupata takwimu sahihi na kuufanya uwe miongoni mwa mikoa itakayofanya vizuri katika zoezi hili la Sensa ambalo hufanyika kila baada ya miaka 10," alisema.

Serukamba alisema makarani na wasimamizi watapewa madodoso hivyo ni muhimu wajifunze mbinu za kuwauliza wananchi ili kuwafanya wawaelewe watakapokuwa wakiwadadisi.

"Kuja mtu unaweza kumuuliza una ng'ombe wangapi akashindwa kueleza pengine akidhani unataka kuja kunyang'anya ng'ombe wao ...hapana ni muhimu kujifunza mbinu za kumfanya mtu akuelewe sababu majibu yenyewe yanatokana na maswali rahisi atakayoulizwa," alisema.

Aliongeza kwa mfano Tanzania inaelezwa ni nchi ya pili katika Afrika kwa kuwa na mifugo mingi baada ya Ethiopia lakini ukiuliza tuna ng'ombe au mbuzi wangapi hakuna anayejua.

Alisema Sensa inakwenda kuleta majawabu yote hayo kinachohitajika ni umakini kwa makarani na wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi walioaminiwa na Serikali kuifanya kazi hiyo kwa umakini na weledi wa hali ya juu.

Naye Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Singida, Mratibu wa Sensa Mkoa wa Singida, Naing’oya Kipuyo, makarani 445 wamehitimu mafunzo yao ya dodoso la Sensa ambalo watahoji majengo na makundi maalum.

Alisema kundi la pili ni la wasimamizi wa maudhui ambao watahoji dodoso la jamii ambao wapo 212 ambao wataendelea na mafunzo kwa siku tatu.

MWISHO

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.