• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba atembelea Vituo vya kulisha watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Posted on: January 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amelishauri Shirika la Kimataifa la Outreach linalo hudumia watoto wanaoishi kwenye Mazingira magumu kuendelea kuwapatia huduma ya chakula na misaada mingine hata baada ya kumaliza kidato cha nne mpaka watakapoingia vyuo vikuu kwa kuwa changamoto walizokuwa nazo awali zinakuwa hazijaisha.

Ushauri huo ameutoa leo alipotembelea vituo vya Outreach International vilivyopo Singida mjini na Manyoni lengo likiwa ni kuona miundombinu ya vituo hivyo na namna watoto wanavyopata huduma tarajiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, akizungumza mara baada ya kuhitimisha ziara yake Wilayani Manyoni kutembelea vituo hivyo vya Shirika la Outreach Internation.

Amelishukuru Shirika hilo kwa kusaidia watoto zaidi ya 1094 ambapo Kituo cha Singida mjini kina idadi ya watoto wapatao 534 na Manyoni 560 kutoka maeneo mbalimbali ambao wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu.

Hata hivyo RC Serukamba amepongeza Shirika hilo kwa namna ambavyo wanawapata watoto hao kupitia kwa wenye Viti wa Vijiji na walimu wa shule jambo ambalo ameeleza kwamba watakuwa wanapata watoto wanaoishi kwenye mazingira hayo na sio ubabaishaji.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Shirika hilo la Outreach Internetional Bw. Mike Wilhelm akitoa maelezo ya awali kwa RC Serukamba amesema kwa sasa wanampango wa kutengeneza vikundi kwa wanafunzi wao waliomaliza kidato cha nne ili kuweza kuwakopesha mitaji kwa ajili ya kufanya  biashara.

Makamu wa Rais wa Shirika la Outreach Internetional Bw. Mike Wilhelm, akitoa taarifa fupi ya Shirika hilo kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati wa ziara yake.

Amesema Shirika hilo mbali ya huduma ya kulisha watoto wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali ambapo wameweza kuchimba visima 58 katika Kata ya Ilunda Wilayani Mkalama, Ujenzi wa nyumba 17 za Walimu katika Kata ya Nkungu, mashule na Zahanati katika jamii ya Wahadzabe.

Aidha amesema watoto hao wamekuwa wakifaulu mitihani yao katika mashule wanayotoka kwa asilimia mia moja kutokana na masomo ya ziada wanayofundishwa katika vituo hivyo.

Hata hivyo Mike amesema amelipokea wazo la RC Serukamba na atalifikisha katika Bodi ya Shirika hilo ili kujadiliwa na kufanyiwa maamuzi.

Wanafunzi wakiwa darasani katika kituo cha Outreach International tawi la Singida mjini

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.