• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba awaagiza Watendaji wa Halmashauri kuhakikisha miradi kukamilika kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Posted on: May 27th, 2023

MKUU wa Mkoa Singida, Peter Serukamba, amewagiza watendaji katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kuhakikisha wanaosimamia miradi inayotekelezwa wilayani humo ikamilike yote kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Aidha, ametoa agizo kwa miradi ya ujenzi wa shule mpya za msingi inayojengwa kwa fedha za BOOST Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lipeleke huduma ya umeme maeneo ya mradi ili kazi ya ujenzi ifanyike usiku na mchana.

Serukamba ametoa agizo hilo baada ya kufanya ziara ya siku mbili kukagua miradi ya ujenzi wa shule mpya za msingi, zahanati, vituo vya afya, mabweni, madarasa na vyoo ambayo Serikali imetoa mamilioni ya fedha kwa ajili ya kuitekeleza.

"Tunaipongeza sana Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeleta fedha nyingi sana kwenye Halmashauri hivyo ambao tumepewa nafasi ya kuwa viongozi kazi yetu ni kuhakikisha fedha hizo zinafanya kazi iliyokusudiwa miradi ikamilike kwa wakati na izingatie 'value for money'," alisema.

Mkuu wa Mkoa alisema moja ya maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Angellah Kairuki, ni kuhakikisha kusiwe na bakaa yaani fedha zinarudi baada ya mwaka mpya wa fedha kwisha badala yake miradi yote inakwisha.

"Mkalama kwenye shule zinazojengwa kwa fedha za BOOST kasi sio nzuri sana ndio maana nimempa maelekezo Mhandisi wa Halmashauri ya  Wilaya ahakikishe kila siku anatembelea miradi na kutoa maelekezo kwa mafundi ili miradi ikamilike Juni 20 mwaka huu," alisema.

Serukamba alisema kuanzia sasa kazi ya ujenzi wa miradi hiyo iwe inafanyika hata siku za Jumamosi ili kukimbizana na muda kwani asingependa kuona baada ya Juni 30 fedha zinarudishwa serikalini kwasababu miradi haijakamilika.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mkalama, James Mkwega, alimhakikishia Mkuu wa Mkoa kwamba miradi yote katika Wilaya hiyo itamalizika kwa muda uliipangwa.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.