• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba awahubiria Madiwani Mkoani Singida uadilifu na ushirikiano.

Posted on: September 6th, 2022

Madiwani wa Halmashauri za Wilaya zote za Mkoa wa Singida wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu na kushirikiana hasa katika miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa maeneo mbalimbali Mkoani hapo ili kuimarisha usimamizi wa watendaji katika Halmashauri zao.

Akiongea katika mabaraza mbalimbali ya Madiwani aliyohudhuria leo Mkoani hapo yakiwemo Manispaa ya Singida, Singida Vijijini, na Mkalama kama sehemu ya kujitambulisha, Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba ameonya tabia ya baadhi ya Madiwani kuwa wakusanya kodi na watoa misamaha ya ushuru katika mageti mbalimbali ya kukagua mazao na kuwataka kusimamia majukumu yao ya msingi ya kuwasimamia watendaji.

Serukamba amesema vitendo ambavyo sio vya kiadilifu vikifanywa na viongozi kama Madiwani vitasabisha kiongozi huyo kushindwa kuwasimamia watendaji wa kazi hata kama watakuwa na makosa katika kazi zao.

"Ukimuomba Mhandisi akupe mifuko miwili ya saruji yeye atachukua mitano na hutaweza kumuuliza, ukikusanya kodi wewe watendaji hawataweza kukuuliza na Diwani hutaweza kumsimamia mwingine ambaye alikusanya kodi pasipo kupeleka benki”. Alisema Serukamba

Akiongelea kuhusu msimu wa kilimo RC Serukamba  ameelekeza kwamba  Madiwani wahakikishe kwamba wakulima wanaongeza eneo la kilimo ikilinganishwa na mwaka jana kwa kuwa Serikali imeendelea kutoa ruzuku za pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu na mbolea.

Aidha Serukamba amewataka wakulima mkoani hapo kuanza maandalizi ya mashamba mapema ili mvua za kwanza zitumike kwa kupandia kwa kuwa uzoefu wa msimu uliopita ulionesha kwamba waliowahi kupanda walipata mazao ikilinganishwa na waliochelewa kupanda.

Hata hivyo RC amesema kwamba Serikali inatumia kiasi kikubwa cha fedha kuagiza mafuta ya kupikia kutoka nchi za nje ambapo ameeleza kwamba Mkoa wa Singida una uwezo mkubwa kuondoa pengo hilo kwa kuongeza eneo la uzalishaji na matumizi ya mbegu bora za kilimo.

Mkuu wa MKoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza na Madiwani pamoja na Watendaja wa Halmashauri ya Wilaya Mkalama 

Akiwa Mkalama Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa eneo hilo kuhakikisha kunajengwa soko la vitunguu ili kuondokana na changamoto ya walanguzi kuwafuata wakulima mashambani.

Aidha amesema kwa kuwaacha walanguzi kuingia mashambani kumesababisha wakulima kutopata faida inayotokana na kazi yao kwa sababu ya ulanguzi unaofanywa huko shambani.

Hata hivyo Serukba ameendeleza kampeni yake ya kuhakisha kila kaya inakuwa na BIMA ya Afya ya CHF iliyoboreshwa ambapo amewataka Madiwani kusaidia zoezi hilo kwamba hata mwananchi ambaye hatakuwa na uwezo kulipa 30,000 watatoa mifugo kwa ajili ya kupata bima hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Singida Vijijini Elia Digha akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Sehemu ya Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Singida Vijijini

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.