• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA AZINDUA JENGO LA UTAWALA HALMASHAURI YA WILAYA SINGIDA DC

Posted on: August 15th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amezindua jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Singida na kuwataka Watumishi wa Halmashauri hiyo kulitunza jengo hilo na kutoa huduma bora kwa Wananchi bila kufanya upendeleo.

Akizungumza na Wananchi na Watumishi leo (Agosti 15, 2023) baada ya kuzindua jengo hilo, alisema  amewataka watumishi wahakikishe wanatoa huduma nzuri kwa wananchi na kutoshiriki vitendo vya kuomba rushwa kutoka kwa watu wanao wahudumia.

Serukamba aliwataka pia Watumishi na Madiwani kila mmoja apewe mti wa kupanda kuzunguka jengo hilo na kuhakikisha anautunza hadi unakuwa ili kutunza mazingira kuzunguka jengo hilo.

"Tutoe huduma nzuri kwa wananchi tusiombe rushwa, pia msitoe huduma kwa upendeleo itakuwa haina maana Serikali imetoa Shilingi bilioni 2.7 kwa ajili ya kujenga jengo hilo halafu huduma zianze kutolewa mbaya.

Aidha, Mkuu wa Mkoa aliwapongeza wananchi waliotoa eneo la kujenga jengo hilo la Halmashauri ambalo litasaidia kutoa huduma kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula, alisema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2020/2021 ilitenga bajeti kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo la utawala ambapo eneo la ujenzi lilipatikana katika kijiji cha Mwahango kata ya Ilongero.

Alisema Halmashauri imekwisha pokea Sh.bilioni 2.7 kutoka Serikali kuu kuanzia mwaka wa fedha wa 2020/2021 hadi 2022/2023 ambapo kiasi kilichotumika hadi sasa ni Sh.bilioni 2.6 ambazo zimetumika kununulia vifaa vya ujenzi, samani za ofisi pamoja na malipo ya mafundi.

Chaula alisema katika mwaka huu wa fedha wa 2023/2024 Halmashauri imetenga Sh.milioni 800 kwa ajili ya kuongezea samani za ofisi, kununua vifaa vya TEHAMA, kukamilisha uzio, eneo la kuegesha magari na uchimbaji wa kisima cha maji baada ya mahitaji kuongezeka.

Alisema wakati wa utekelezaji wa mradi huo, zilijitokeza changamoto zilizosababisha jengo la utawala kuchelewa kukamilika ambazo ni kuaribika kwa saruji wakati wa ujenzi wa miradi ya COVID 9, kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi na kukosekana kwa maji.

MWISHO

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.