• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA AFUNGA MGODI ‘SEKENKE NAMBA MOJA’ KUPISHA UCHUNGUZI

Posted on: December 14th, 2019

MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amefunga kwa muda mgodi wa ‘sekenke namba moja’  uliopo wilaya ya Iramba mkoani hapa kama tahadhari kupisha uchunguzi wa kina na kitaalamu kubaini chanzo kilichosababisha kutitia ghafla kwa sehemu kubwa ya udongo eneo hilo na kusababisha taharuki kwa wananchi.

Akizungumza kupitia mkutano wa hadhara kwenye eneo hilo la tukio, Dkt. Nchimbi alisema tangu kutokea kwa tukio hilo lisilo la kawaida (juzi), kila alipojaribu kuhoji nini hasa kimesababisha eneo hilo kuzama, na kilichozama hapo ni udongo pekee au kuna watu wamefukiwa? Lakini mpaka sasa maelezo anayopokea ni kugongana-gongana.

 Alisema baadhi ya wamiliki wa maeneo hayo walimweleza kuwa kuzama (kutitia) huko kwa udongo kumesababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha. Wakifafanua kwamba maji ya mvua yalitiririka na kukutana na nyufa, na hatimaye kulainisha udongo uliokuwa umeshikana na nguzo, na kupelekea udongo kuachia na kutitia.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi, akizungumza na wafanyakazi wa Migodi ya Sekenke (hawapo pichani), muda mfupi kabla ya kuufunga mgodi wa sekenke namba moja, uliopo halmashauri ya wilaya ya Iramba, mkoani Singida

“Nikiwa Mkuu wa mkoa huu, tena mama ambaye ni lazima nisimame katika kuhakikisha usalama na mazingira mazuri ya kunufaika na haya ambayo Mwenyezi Mungu ametupa, kuanzia leo Disemba 12, 2019 ninapafunga hapa, ninafunga mgodi namba moja kupisha uchunguzi wa kina mpaka pale mtakapopewa taarifa,” alisema Nchimbi na kuongeza;

“Ninafunga namba moja ila namba mbili iendelee. Nafunga sekenke namba moja hadi pale wataalamu wa madini watakapokuja kufanya uchunguzi kubaini kama chanzo cha kutitia huko ni mvua kweli, na kama kuna madhara mengine ikiwemo vifo,”

Aidha, Nchimbi akitoa tathmini yake binafsi juu ya alichokibaini kwenye eneo la tukio, alisema kilichosababisha kutitia kwa udongo huo ni ubinafsi, ni tamaa, uroho wa kutaka kupata fedha kwa haraka, na watu kukosa hofu ya Mungu, huku akisisitiza kuwa watu wa aina hiyo ndio waliolipua zile nguzo zinazoshikilia pale kwa makusudi.

“Kuna nguzo pale tangu enzi za utawala wa Mjerumani zinazoshikilia, Mkoloni huyu pamoja na nguvu zake, pamoja na uwezo wake, na kwa kutambua eneo hilo la nguzo kuna dhahabu alisema endapo nitalipua hizi nguzo basi huu mgodi hautakuwepo, na hakuwahi kufanya hivyo,” alisema Nchimbi

Alisema anasubiri majibu ya wataalamu, ila sababu ya kwamba mvua imesababisha haimridhishi, kutokana na huko nyuma kuwapo na mvua nyingi zikiwemo za El-Nino lakini tukio kama hilo halikuwahi kutokea, huku akihoji kama ni mvua mbona sekenke namba 2 haijadhurika, mpaka sasa pako salama. 

Aliwataka wafanyakazi hao kuwa na subira kupisha uchunguzi ili kubaini kwa haraka kama ni mvua kweli, na kama sababu itakuwa ni mvua basi atalazimika pia kuufunga mgodi huo kusubiri mpaka pale msimu wa mvua utakapomalizika. Aidha alisema kama ikibainika atakuwa amesababisha mtu basi atatamani ikiwezekana afutiwe kabisa leseni ya kujishughulisha na madini.

Alisema mara kadhaa zinapotokea dhoruba kama hizo wanaokufa huwa ni wafanyakazi, huku wamiliki wa migodi na miduara hiyo wakiendelea kuwa salama. Alisema mathalani leo (juzi) alipokuwa akiongea na wamiliki hao aliwauliza kwanini msiwe mnatangulia kufa ninyi? Maana wanafanya upuuzi sababu wao hawaingii huko.

Moja ya vitendea kazi katika mgodi wa Sekenke.

“Nataka niwahakikishie wafanyakazi Rais Magufuli anawapenda sana, na eneo hili lote mlimchagua kwa kura nyingi, fursa hii ya madini haikutolewa na serikali au kuruhusiwa ili watu wafe hapana! Tunataka madini yetu yasigeuke chanzo cha huzuni na maafa, bali yatuletee amani, furaha, maisha marefu kwa vizazi na vizazi…na hii ndiyo furaha ya taifa lolote lile ambalo linajipenda,” alisema Dk Nchimbi

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba ambaye eneo hilo ni sehemu ya jimbo lake, aliomba wananchi watoe ushirikiano wakati wote zoezi la ukaguzi litakapokuwa likiendelea, na kuwataka kuchukua tahadhari kuepuka athari nyingine inayoweza kujitokeza hata wakati wa uokoaji.

“Pia ninaomba tupewe ruhusa kwa wale wenye mitambo yao hapo nje na wana mawe ambayo tayari wamekwisha yachimba basi waendelee kusafisha wakati taratibu nyingine zikiendelea…tupewe ruhusa ya kusafisha na sio kuchimba,” alisema Nchemba

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.