• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Singida Peter Serukamba akabidhiwa ofisi rasmi, atoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri mkoani humo.

Posted on: August 4th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba  leo ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa huo kuhakikisha kwamba kila Mwananchi Mkoani hapo anakuwa na kadi ya afya kama hatua mojawapo ya kuboresha za Wananchi hao.

Agizo hilo amelitoa leo wakati wa makabidhiano ya ofisi baina yake na  aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Binilith Mahenge hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo.

Amesema Serikali imetoa fedha nyingi kujenga vituo vya Afya Zahanati na Hospitali lengo likiwa ni kutoa huduma za Afya kwa wananchi hivyo ni muhimu kuhakikisha wananchi wanapata Bima za Afya ili waweze kupata huduma hizo kwa urahisi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba   akizungumza na Watumishi wa Umma mkoani Singida mara baada ya kukabidhiwa ofisi rasmi katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

'"Moja ya mambo ambayo nitaanza nayo katika kazi yangu ya Mkuu wa Mkoa ni kuhakikisha kila mwananchi anapata Bima ya Afya, ambapo gharama yake ni sawa na kuku watatu"

Alisema Serukamba swala la Afya ni mtaji mkubwa sana kwa wananchi katika kuleta maendeleo hivyo ni jukumu la kila kiongozi kuhamasisha    wananchi kupata kadi ya afya.

Sambamba na hilo RC Serukamba ameagiza Halmashauri hizo kuongeza vyanzo vya  ukusanyaji wa mapato na kuacha kukadiria  viwango vidogo vya makusanyo huku akiongea kuacha kuangalia asilimia na badala yake waangalie wingi wa fedha.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri hizo kuhakikisha mapato yanaongezeka kwa kuwa vyanzo vipo ila havijatiliwa mkazo.

Aidha RC Serukamba amezitaka Taasisi zinazohusika na Barabara zikiwemo Tanroads na TARURA kwa kushirikiana na Halmashauri kuhakikisha mji unakuwa safi hasa katika Barabara zetu na kuzuia utupaji wa taka kiholela.

Amesema katika kipindi cha wiki moja anataka Mazingira  yawe safi katika Barabara zote za lami pamoja na sehemu za mjini.

Kwa upande wake Dkt Binilith Mahenge aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo aliwashukuru Watumishi na wananchi wote kwa ushirikiano waliompa wakati wa uongozi wake na kuwasihi kutoa ushirikiano mkubwa kwa Mkuu wa Mkoa wa sasa.

Katika taarifa yake Dkt. Mahenge amemueleza Mkuu wa Mkoa kwamba shughuli kubwa inayokaribi Mkoani hapo ni msimu wa kilimo ambapo ameeleza kwamba wananchi wanajiandaa kwa msimu wa kilimo na mpango ulikuwa ni kugawa mbolea za ruzuku baada ya kuwasajili wakulima.

Amesema Singida ina wananchi na watumishi ambao ni  wachapakazi na wanaopenda maendeleo hivyo anaamini mafanikio makubwa yanaweza kupatikana.

Baada ya makabidhiano hayo RC Serukamba alitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Hospitali ya wilaya ya Ikungi, Veta, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Singida na Hospitali ya Mkoa Mandewa.

MATUKIO KATIKA PICHA

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na watumishi wakati wa makabidhiano

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza na watumishi wakati wa makabidhiano

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko akizungumza wakati wa hafla ya mapokezi na makabidhiano ya ofisi baina ya Mkuu wa Mkoa  Peter Serukamba na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Dkt. Binilith Mahenge iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano mkoani hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (Kushoto) wakati wa ziara yake ya kukagua Hospitali ya Wilaya ya Ikungi 

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.