• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA – TUTAKWAMUA HARAKA UJENZI WA MAJENGO YA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SINGIDA ‘MANDEWA’ ULIOKWAMA ILI WANANCHI WAWEZE KUPATA HUDUMA ZA AFYA.

Posted on: June 3rd, 2024

Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego ameahidi kushughulikia kwa haraka mkwamo wa ujenzi wa majengo Matatu (3) katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida iliyopo Kata ya Mandewa katika Manispaa ya Singida, jengo la ghorofa Tatu linalotarajiwa kutoa huduma za kibingwa ikiwemo upasuaji wa mifupa, wodi za watoto, huduma za wagonjwa mahutututi, maabara na huduma za ufamasia.

Jengo hilo la ghorofa Tatu ujenzi wake ulianza mwaka 2014 na kusimama kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo Mkandarasi aliyekuwa anajenga jengo hilo kusimamishwa kuendelea na ujenzi kutokana na uwezo mdogo katika utekelezaji wa mradi huo.

RC Dendego ametoa kauli hiyo katika kikao na Watumishi wa Hospitali hiyo cha kusikiliza  kero na kukagua majengo ambayo ujenzi wake umesimama na kusisitiza kuwa  atalibeba jambo hilo na kulifanyia kazi ili ujenzi huo uweze kuendeleo na kukamilika kwa haraka lengo likiwa ni kuongeza utoaji wa huduma za matibabu kwa wananchi karibu na maeneo yao.

“Mimi ni Muumini ya Namba Moja kwa kila jambo hivyo nataka Hospitali hii ya Rufaa ya Mkoa iweze kushika Namba 1 nchini na Dunia kwa ujumla kwa utoaji huduma za kiwango cha juu za afya kwa wananchi kwani Hospitali nyingine wanaweza kwa nini sisi tushindwe na Serikali imewezesha vifaa na Watumishi wapo” Amesisitiza RC. Halima Dendego.

Kuhusu Watumishi wanaojitolewa kwa muda mrefu bila kupata ajira, Mkuu huyo wa mkoa ameutaka Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kumpatia orodha ya Watumishi wote wanajitolewa lakini hawajapata ajira ili aweze kuwasaidia katika ngazi husika.

Hata hivyo, Mhe. Dendego amewapongeza Watumishi hao kwa kufanya kazi kwa bidii bila kukata tamaa kutokana na kutopatiwa ajira na kusisitiza kuwa jambo hilo atalishughulikia ili watumishi hao waweze kupata ajira za kudumu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida Martha Mlata, amewasisitiza Watumishi wa Hospitali mkoani humo kuendelea kuchapa kazi bila kuchoka kwa viwango vya juu kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita inawajali na itaendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili kwa muda muafaka.

Naye, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida Dkt. David Mwasota ameishukuru Serikali kwa kuwa bega kwa bega na Watumishi wa afya ikiwemo kuwapatia vitendea kazi vya kisasa na kuboresha maslahi yao hivyo jukumu lao kubwa ni kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi ili wasiende mikoa mingine kufuata huduma hizo za afya.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida Dkt. David Mwasota, akitoa taarifa ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida iliyopo Kata ya Mandewa Singida Mjini. Juni 3, 2024

Ukaguzi wa Majengo ukiendelea

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.