• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERIKALI IMETOA BURE MBEGU NA VIUATILIFU KWA AJILI YA KILIMO CHA PAMBA KWA MKOA WA SINGIDA.

Posted on: November 7th, 2017

  Serikali imeahidi kutoa bure pembejeo za kilimo kwa wakulima mbali mbali wa zao la pambamkoani Singida kuanzia msimu huu wa kilimo ikiwa ni moja ya juhudi za kuhamasishana kufufua kilimo hicho mkoani hapa.  

MkurugenziMkuu wa Mamlaka ya Bodi ya Pamba nchini, Marco Mtunga ameeleza hayo juzi katikavijiji vya Kinyangiri na Lyelembo wilayani Mkalama katika siku ya kwanza yaziara yake ya siku mbili kuhimiza Kilimo cha pamba mkoani Singida. 

Kwamujibu wa Mkurugenzi huyo, Kampuni ya Biosustain iliyopo mjini hapa imepewajukumu la kuleta na kusambaza mbegu na madawa yote yahusuyo kilimo cha pambabure na kwamba gharama ya pembejeo hizo italipwa na Serikali. 

Kutokanana hilo, Mkurugenzi huyo amewataka Wakulima kutumia vyema fursa hiyo kwa kulimamashamba makubwa zaidi lakini pia kwa kuzingatia tija na ubora wa pamba. 

Amesemakuwa Wakulima wataweza kufanya hivyo tu iwapo pia watawatumia kikamilifuwataalamu wao wa kilimo na kufuata Kanuni na Taratibu za kilimo bora. 

“Mmepewaupendeleo maalum, kazi yenu sasa ni kulima tu, malipo ya mbegu na viuatilifuvyote italipwa na Serikali. Hapa hakuna kisingizio cha kushindwa kulima”, amesemaMtunga na kuongeza;

“Pandenivizuri ili wakati mnatumia dawa, kiwango kikubwa cha dawa kisipotee bure maanakama hukupanda kwa mstari lazima kutakuwa na ugumu wa kupulizia mimea yako.Jengeni utamaduni wa kuwatumia wataalamu wa kilimo kama ilivyo kwa wafugajimifugo yao inapopatwa na maradhi”.  

Aidha,amewataka wakulima wa zao hilo kuhakikisha wanang'oa masalia yote ya misitu yapamba na kuichoma moto kwa kuwa, kwa kuacha kufanya hivyo wanaruhusu waduduwaliomo kwenye masalia kuendelea kunenepeana na hivyo kuhatarisha mazao mapyayanayopandwa.  

Mkurugenzihuyo amewasihi wakulima kuacha kuchanganya kilimo cha pamba na mazao mengineakisema kuwa tafiti zinaonesha pamba iliyochanganywa na mazao mengine hutoavitumba vitatu tu ikilinganishwa na vitumba 10 kwa kilimo cha pamba iliyolimwapeke yake. 

Wakulimawa zao hilo wamemueleza Mkurugenzi huyo kuwa, moja ya sababu za kushuka kwauzalishaji pamba kwenye maeneo yao ni pamoja na bei kuwa ndogo kwa kisingiziocha Soko la Kimatafa kushuka na kuchezewa mizani wanazotumia kupima mazao yao,hali inayowapunja kimapato.  

Hatahivyo, wamejibiwa kuwa suluhisho la kuchezewa mizani lipo mikononi mwao ilimradi tu wajenge tabia ya kuhoji mara moja wanapoona mambo yanaenda isivyobadala ya kusubiri hadi siku ya vikao. 

Wakatihuohuo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewataka watendaji wote waserikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Singida kulima ekari moja ya pambakila mmoja ili kuamsha hamasa kwa wananchi wengine.

DktNchimbi ameongeza kwa kuwataka watendaji hao kuliweka zao la pamba kama ajengakatika vikao vyao, huku akiwataka viongozi wa dini na vikundi vya kwayakuonyesha mfano kwa kulima vizuri pamba.

Ameongezakuwa vijana wanaocheza vijiweni ‘pooltable’ waache mara moja na kujikita katikakilimo cha pamba kwa kuwa ni chanzo kikubwa na cha uhakika cha kujipatia fedhana hivyo kuchangia kukuza uchumi. 

Aidhaamewataka wakulima wa pamba kuwasikiliza wataalamu na sio kupanda kwa mazoeahuku akishauri kuwa mikutano yote inayohusu kilimo cha pamba ifanyike katikamashamba ya wakulima.

DktNchimbi ameeleza kuwa kauli mbiu mpya ya kilimo cha pamba kwa Mkoa wa Singidani, ‘Singida Mpya, kwa Pamba yenye Tija’. 

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.