• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Serikali Itatoa Mbegu Za Alizeti Kwa Wakulima – Bashe

Posted on: October 12th, 2021

Serikali imejipanga kuinua uzalishaji wa zao la alizeti katika Mkoa wa Singida kwa kuwakopesha wakulima mbegu aina ya Record ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kuondoa uhaba wa mafuta ya kula ambao umekuwa ukijitokeza kila mwaka.

Akiongea wakati wa ziara yake leo Wilayani Singida Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Hussein Bashe amesema wataikabidhi Halmashauri hiyo tani 100 za mbegu za alizeti standerd seed ambapo wakulima watakopeshwa.

Mkopo huo wa mbegu za ruzuku zinazogharimu kiasi cha shilingi 3500 kwa kilo MOJA watazirejesha kwa Halmashauri husika baada ya kuvuna mazao yao na kuyauza. Alibainisha Bashe.

Naibu Waziri huyo amefafanua kwamba wakati wa ugawaji wa mbegu hizo maafisa kilimo wahakikishe kila mkulima anaandika jina, Kijiji alichotoka, namba ya simu ukubwa wa shamba alilolima na kiasi cha mbegu alichopewa na kusaini.

Aidha Mhe. Bashe ameagiza Halmashauri kuhakikisha makampuni yote yatakayonunua mbegu za alizeti kuhakikisha wanatoa huduma za ugani kwa wakulima watakao wazalishia na kuhakikisha eneo lililopata huduma hizo linauza kwa makampuni husika.

Amewaomba viongozi wa siasa kuhakikisha wanasimamia ugawaji wa mbegu kwa wakulima, usimamizi wa mashamba pamoja na makampuni yatakayoonesha nia ya kushirikiana kwa namna yeyote na wakulima ili kusaidia kuongeza uzalishaji wa alizeti.

Hata hivyo akawataka Maafisa ugani kuhakikisha msimu ujao wa kilimo wa mwaka 2022/23 wanakuwa na taarifa za kila Kata kuhusu aina ya mazao yanayostawi eneo hilo na aina ya mbolea itakayohitajika ili wakulima waweze kulima zao zaidi ya moja.

Wizara ya kilimo itatoa vitendela kazi vikiwemo mashine za kupimia udongo kwa kila Hamashauri ili kurahisisha zoezi hilo, alieleza Naibu Waziri.

Amesema wakulima wanapaswa kulima mazao mbalimbali yenye thamini kubwa katika masoko ya ndani na nje ya nchi kwa lengo la uimarishaji wa usalama wa chakula kwa kila mkulima na kuongeza kipato alisistiza Mhe. Bashe

Hata hivyo Naibu Waziri alieleza kwamba Wizara ya kilimo kupitia Wakala wa mbegu za kilimo (ASA) imeweka mikakati ya kuzalisha mbegu nyingi za kisasa katika msimu wa 2022/23 ili kurahisisha upatiakanaji wa mbegu.

Awali Naibu Waziri huyo ameahidi kuwatuma wataalamu wa umwagiliaji kutoka wizarani waungane na wenzao wa mkoani wakafanye tathmini katika skimu zote za Mkoa wa Singida na kuchagua baadhi ambazo zitakarabatiwa kwa asilimia miamoja ili kuleta matokeo makubwa katika kilimo.

Amesema mkoa mzima wa Singida una skimu za uwagiliji zenye jumla ya ukubwa wa hekta 3,450 lakini hekta zinazo tumika ni 100 tu ambazo ni chini ya asilimia kumi jambo ambalo haliewezi kuleta mabadiliko makubwa ya katika kilimo.

“Lazima tuondokane na kilimo cha kubahatisha, ili tuweze kukifanya kilimo kiwe cha ki biashara ni lazima tuingie kwenye kilimo cha umwagiliaji na tutafute namna ya kutunza miuondombinu kwa kulipa tozo kidogo itakayosaidia kurekebisha miundombinu hiyo”. Alisema Bashe.

Katika ziara hiyo Naibu waziri aliweza kutembelea skimu ya uwamgiliaji iliyoko Kijiji cha Msikii Kata ya Mughamo yenye hekta 150 zinazofaa kwa umwagiliji na Kijiji cha Msange chenye hekta 1,400 ambapo chanzo cha maji ni bwawa lianalohitaji ukarabati na uchimbaji wa visima .

Akiwa maeneo hayo Naibu waziri huyo ameongea na wakulima wa vitunguu na mahindi ambapo kupitia wakala wa mbegu ASA ameahidi kuwaletea mbegu ya mahindi aina ya stuka waifanye kama majaribio lengo likiwa ni kuwafanya wakulima hao kulima kilimo cha mazao mbalimbali.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Mhandisi Paskasi Muragili amesema Hamashauri hiyo imejipanga kikamilifu kutekeleza maagizo ya Serikali kuanzia yote yaliyotolewa na Waizri Mkuu yanayohusu uendelezaji wa zao la alizeti na mkakati wa kuongeza uzalishaji wa mafuta nchini.

Amesema wilaya ya Singida mwanzoni walikuwa na wakulima 8,546 wa alizeti ambao walilima hekta 21,000 na kuvuna tani 36,222 lakini baada ya maagizo ya Serikali wametoa elimu na hamasa wakulima 21,000 wamejiorodhesha kulima hekta 38,000 kwa wakulima wadogo na Taasisi 438.

Amesema wilaya hiyo inategemea kuzalisha tani Zaidi ya 94,000 kwa msimu ujao ambapo ni mara mbili zaidi ya msimu uliopita.

Mtendaji wa Kata ya Mughamo Katika Halmashuri ya Wilaya ya Singida Bw. Clement Njou akisoma taarifa fupi ya shughuli za kilimo katika Kata hiyo.

Mkuu Wilaya ya Singida Paskasi Muragili (kulia) akiwa ameshikili zawadi ya miwa walipewa na wanakijiji cha Msikii, wapili kutoka kulia ni Naibu Waziri Bashe

Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Hussein Bashe (kulia) akiwa katika shamba la mbegu za vitunguu

Muonekano wa eneo la bonde lililopo Kata ya Mughamo katika Halmashuri ya Wilaya ya Singida

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.