• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Serikali kuendeleza kutoa matibabu Bure kwa Wazee

Posted on: October 1st, 2021

Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa matibabu kwa Wazee bila malipo, upatikanaji wa dawa Hospitalini  na uwepo wa dirisha maalum kwa ajili ya Wazee ili kuwaenzi na kuwaondolea usumbufu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa  wilaya ya Singida Mjini Mhandisi Paskasi Muragili kwaniaba ya Mkuu wa mkoa wa Singida wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wazee Duniani yaliyofanyika mjini Singida.

 Amesema Serikali itaendelea kutoa huduma kwa wazee pasipo kuchangia gharama za matibabu na kuboresha changamoto ambazo zimejitokeza katika utoaji wa huduma hiyo kwa kundi hilo.

 "Sisi sote ni mashahidi wa utolewaji wa huduma za Afya bila malipo kwa Wazee wote. Nitoe wito kwenu kufika kwenye vituo vya huduma za Afya vya Serikali ili kupatiwa huduma bila kuchangia gharama za matibabu".

Aidha Mkuu huyo wa wilaya amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kuendelea kuwachangia wazee wasio na uwezo na kuwaunganisha kwenye Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF) na wale wenye uwezo wa kujiunga wenyewe amewahamasisha wajiunge ili kuendelea kuboresha huduma za Afya.

Awali Mwenyekiti wa umoja wa Wazee hao SAWATA Bw. Ramadhani Juma Moghu ameishukuru Serikali kwa hatua walizoendelea kuzichukua katika kuimarisha Sekta hasa kwa wazee.

Akijibu hotuba ya wazee hao Mkuu huyo wa wilaya amewataka Maafisa maendeleo ya jamii wa kila Halmashauri kuwashauri wazazi  ambao watoto wao wanaolelewa na wazee kuona umuhimu wa mtoto kuishi na mzazi ili  kuwapunguzia majukumu.

Amesema Wazee wengi wameachiwa watoto na watoto wao au wajukuu. Malezi ya watoto hao ni jukumu la wazazi wao hivyo ni vema tukawaelimisha watoto na wajukuu zetu juu ya umuhimu wa malezi ya Wazazi kwa watoto. Alisistiza Muragili

 "Kwa kuwa kila Halmashauri kuna Ofisi za Ustawi wa Jamii niwaombe mfike ili wazazi hawa waweze kuwajibika kama Sheria ya Mtoto Na. 21 ya Mwaka 2009 inavyoelekeza".

“Nitoe shukrani kwa viongozi wa Baraza la Wazee mkoa na Viongozi wa SAWATA katika kufanya maandalizi na kufanikisha maadhimisho haya.  Aidha, nazishukuru Taasisi zote zilizoweza kutoa michango yao ya hali na mali katika kuwezesha maadhimisho haya”.  Alimalizia Muragili.

Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Mhandisi Paskasi Muragili (kulia) akitembalea banda la Wazee wajasiriamali katika 

maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika leo mkoani Singida

Mwenyekiti wa umoja wa Wazee hao SAWATA Bw. Ramadhani Juma Moghu akisistiza jambo wakati wa maadhimisho hayo 

Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Mhandisi Paskasi Muragili (kulia) akikabidhi Mwongozo wa majukumu ya Mabaraza ya Wazee ngazi ya vijiji, mtaa, kata, wilaya na mkoa na Taifa kwa viongozi wa Mabaraza wakati wa madhimisho hayo

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwalimu Dorothy Mwaluko (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa umoja wa Wazee hao (SAWATA) muda mfupi kabla ya kuanza kwa hafla ya maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika leo mkoani Singida 

Burudani zikiendelea

Picha ya pamoja

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.