• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERIKALI YAREJESHA UTARATIBU WA HATI PUNGUZO ILIYOBORESHWA KWA KUGAWA VYANDARUA VYENYE VIUATILIFU.

Posted on: July 8th, 2017

   Serikali imerudisha utaratibu wa kugawa vyandarua vyenye viuatilifu kwa akina mama wajawazito na watoto ambao wanapatiwa chanjo ya surua kupitia vituo vya kutolea huduma za afya ya uzazi na mtoto ambapo utaratibu huo utaanza rasmi mwezi Agosti mwaka huu.

Afisa Muuguzi kutoka Wizara ya Afya Epifania Malingumu amewaambia wajumbe wa mkutano wa uelimishaji juu ya mpango endelevu wa ugawaji vyandarau vyenye viuatilifu vya mda mrefu kuwa kwa sasa vyandarua hivyo havitapatikana katika maduka kama ilivyokuwa kwenye utaratibu wa ‘hati punguzo’ ya zamani.

Malingumu amesema hapo awali vyandarua vyenye viuatilifu vilikuwa vikitolewa kwa mfumo wa hati punguzo ambapo mama mjamzito alikuwa anatakiwa kutafuta maduka ya mawakala wa vyandarua hivyo mara baada ya kupatiwa hati hiyo katika vituo vya kutolea huduma ya afya ya uzazi.

“Utaratibu wa hati punguzo wa zamani ulikwisha muda wake mwaka 2014, akina mama walikuwa wanapata changamoto katika kutafuta mawakala wa vyandarua lakini utaratibu mpya ni kwamba mama mjamzito au mwenye mtoto mchanga atapewa chandarua chenye viuatilifu palepale atakapokuwa katika vituo vya kutolea huduma za afya ya uzazi” amesema.

Ameongeza kuwa mama atapewa chandarua katika hudhurio la kwanza la kliniki ambapo takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 98 ya wajawazito huhudhuria kliniki angalau mara moja pia vyandarua hivyo vitatolewa kwa idadi ya watoto ambao mama atakua amejifungua kwa wakati huo.

Kwa upande wake Mratibu wa zoezi la ugawaji vyandarua nchini Yusufu Mwita amesema vyandarua vyenye viuatilifu ni nyenzo mojawapo ya kupambana na ugonjwa wa maralia endapo kila mwananchi atazingatia kuvitumia kwa ufanisi.

Mwita amesema kwa mkoa wa Singida kumekua na ongezeko la maambukizi ya Ugonjwa wa maralia kutoka asilimia 0.2 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 5.5 kwa mwaka 2016 licha ya vyandarua 954,644 kugawiwa mkoani hapa kwa mwaka 2016.

Ameongeza kuwa mkakati wa ugawaji vyandarua umelenga kuwafikia asilimia 85 ya watanzania wote ifikapo 2025 na kuutokomeza ugonjwa wa maralia kwa kushirikisha mbinu mbalimbali ikiwemo kupulizia dawa ya ukoka ili kuthibiti mazalia ya mbu pamoja na kuhakikisha matibabu sahihi ya ugonjwa wa maralia yanatolewa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amesema Maralia inakuwepo kutokana na kwamba Mkoa wa Singida sio kame una maji ya kutosha hivyo kusababisha mbu kuzaliana kwa wingi.

Dkt. Nchimbi amesema mikakati iliyopo ni mizuri ila inatakiwa iende sambamba na mikakati mingine ya kupambana na ugonjwa wa maralia kwa kuwa ni ugonjwa ambao hupoteza nguvu kazi ya taifa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.