• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Serikali Yatakiwa Kuendelea Kutoa Elimu Kwenye Vikundi

Posted on: January 20th, 2022

Wasimamizi wa Vikundi vya Vijana wajasiriamali wadogo wadogo mkoani Singida wametakiwa kuvishauri na kuvisaidia vikundi hivyo kwa kuangalia mipango kazi yao kabla ya kuwakopesha ili fedha watakazozipata waweze kuzitumia vizuri na kuwaletea maendeleo.

Maagizo hayo yametolewa Januari 20, 2022 na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida  Alhaji Juma Kilimba alipokuwa akikagua kikundi cha vijana kilichopo Iguguno katika wilaya ya Mkalama  kinachofahamika kwa jina la Iguguno Youth Group ambacho kinajishughulisha na ufatuaji wa matofali na ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Ziara hiyo ya kamati ya siasa imeingia siku ya pili ikiwa na lengo la kukagua miradi iliyojengwa kwa fedha za uviko 19, fedha zitokanazo na tozo za miamala ya simu pamoja na mapato mbalimbali ya Halmashauri.

Aidha Alhaji Kilimba amesema vikundi vyote vinavyokopeshwa fedha za Serikali ni lazima vilelewe vizuri ili vikomae na kufikia kikomo na kupisha vikundi vingine viweze kukua hivyo akawataka Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa na Wilaya kuhakikisha wanawashauri na kuwaongoza hasa katika kipidi wanapowakopesha fedha ili waweze  kufikia malengo yao.

“Ni lazima elimu itolewe kwa wanakikundi wajue namna ya kuandika mahesabu ya mapato na matumizi wapate elimu juu ya namna ya kupambana na majanga yanayoweza kujitokeza katika biashara zao pamoja kuendeleza mitaji  iweze kukua” alisema Bwana Kilimba.

Hata hivyo ameitaka Serikali kuvisaidia vikundi hivyo kupata masoko ya bidhaa wanazozalisha kama sehemu ya kuwaunga mkono hali itakayosaidia kushawishi vijana wengine kujiunga au kuanzisha vikundi mbalimbali vyenye kuongeza ajira na vipato kwa vijana.

Awali akisoma taarifa ya kikundi hicho Bi Winifrida Innocent katibu wa kikundi amesema Halmashauri ya Mkalama iliwakopesha fedha kiasi cha Sh. Milioni 15 ambazo zilitumika kununua baadhi ya vifaa kama mashine ya umeme na inayotumia mikono kwa ajili ya kufyatulia matofali, vibao pamoja na sement.

Aidha ameishukuru Halmashauri ya Mkalama kwa kuwa imekuwa ikiwasaidia ushauri na wataalamu ambao wamekuwa wakiwatembelea mara kwa mara.

Hata hivyo ziara hiyo ya Kamati ya siasa imefanyika katika wilaya mbili za Mkalama pamoja na Iramba ambapo walikagua miradi ya maji, madarasa  na kituo cha afya  ambapo kamati hiyo  imeridhishwa na ujenzi ulivyofanyika na namna ambavyo watoto wamekuwa wakiendelea kusajiliwa katika mashule hayo.

Hata hivyo Mwenyekiti amesisitiza utunzaji wa miradi hiyo ili iweze kusaidia vizazi vijavyo hasa katika vyumba vya madarasa na thamani zake wakati kwenye miradi ya maji akiwataka wataalamu kuhakikisha maji yanasambazwa karibu na makazi ya watu.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Dkt. Mahenge Atangaza Fursa kwa Wawekezaji Mkoani Singida

    May 14, 2022
  • Madiwani Watakiwa kushiriki kikamilifu zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi na Posti Kodi Wilayani Manyoni

    May 11, 2022
  • Taasisi binafsi zatakiwa kuonesha ushirikiano katika uwekaji wa Anwani za Makazi Manispaa ya Singida.

    May 10, 2022
  • Watendaji wa Makiungu, Mungaa Watakiwa kufanya "Data Cleaning" Katika zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi.

    May 09, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.