• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Serikali yatoa power benk 200 Mkoani Singida kwa ajili ya vishkwambi vya Makarani wa Sensa.

Posted on: August 24th, 2022

Serikali imetoa power benk 200 katika maeneo ambayo yanachangamoto ya ukosefu wa umeme Mkoani Singida kama sehemu ya utatuzi wa changamoto ya kuishiwa chaji kwa vishikwambi ambavyo vinatumiwa na Makarani wa Sensa ya watu na Makazi ya 2022.

Akiongea baada ya kuwatembelea Makarani hao katika Manispaa ya Singida, Singida Dc na Wilaya ya Mkalama Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema Serikali imetoa Power Benk hizo kwa kuwa jana uzoefu umeonesha baadhi ya maeneo Makarani kupata changamoto baada ya vitendea kazi vyao kumaliza chaji kabla ya muda.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba (kushoto) akizungumza na Karani wa Sensa wakati wa ziara yake Singida Vijijini

Amesema kutokana na ukaguzi alioufanya kupitia Makarani wapata Tisa ameona zoezi linaendelea vizuri na kuna kila dalili ya kumaliza zoezi hilo ndani ya muda na kila mwananchi kufikiwa.

RC Serukamba amawaomba wananchi wa Mkoa huo kutoa ushirikiano mkubwa kwa Makarani ikiwemo kuwaruhusu kuchaji vishikwambi vyao kwenye makazi yao wakati wakiendelea kuhesabu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili amesema zoezi linaendela vizuri na haijatokea changamoto yoyote kwa kuwa wataalamu wa tehema wamekuwa karibu na Makarani kwa ajili ya utatuzi wa changamoto yoyote itakayojitokeza.

Aidha amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kwamba kwa upande wa Wilaya ya Singida wanategemea mafanikio makubwa kama walivyotegemea.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili (kushoto) akizungumza wakati wazira ya Mkuu wa Mkoa huo kujionea hali inavyoendelea kwenye zoezi la Sensa ya Watu na Makazi mkoani hapo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo ameeleza kwamba changamoto ya kuishiwa chaji imejitokeza kwa Makarani wa Wilaya hiyo kwenye vijiji ambavyo havijapata huduma ya umeme.

Hata hivyo amemuomba Mkuu wa Mkoa katika Power benk zilizokuja Wilaya hiyo ipewe kipaumbele kwa kuwa pamoja na changamoto ya umeme kwa ajili ya kuchaji lakini bado kuna umbali wa nyumba hadi nyumba.

Kizigo amewataka wananchi ambao bado hawajahesabiwa kuhakikisha kuendelea kuwa na subira kwa kukuwa katika kipindi cha siku Tano zilizobaki watahakikisha kila mwananchi anafikiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ziara ya Mkuu wa Mkoa huo kujionea maendeleo ya zoezi la Sensa katika mkoa wa Singida.

Aidha Mratibu wa Sensa Mkoa wa Singida Naing'oya Kipuyo amekiri kupokea power benk hizo ambazo zitakuwa msaada mkubwa kwa Makarani waliyopangiwa Vijijini ambapo hakuna Umeme.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.