• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERIKALI YATOA ZAIDI YA SH.524 MILIONI KUJENGA BARABARA WILAYANI IRAMBA

Posted on: December 20th, 2021

SERIKALI imetoa Sh.524,448,800 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Shelui-Tintigulu yenye urefu wa kilomita 7.3 katika Kata ya Shelui wilayani Iramba mkoani Singiga.

Hayo yalisemwa na Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Iramba, Evance Kibona wakati akitoa taarifa mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa, na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Ummy Mwalimu katika ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kukagua miradi ya maendeleo aliyoifanya wilayani humo leo.

Kibona alisema mradi huo unatekelezwa kwa fedha za tozo kutoka Serikali Kuu na ujenzi wa barabara hiyo unafanywa na Kampuni ya M/s Jp Traders Limited ya jijini Dar es Salaam na kuwa ujenzi huo ulianza rasmi Desemba 11, 2021 na unakadiriwa kukamilika Juni 10 mwakani.

"Mradi huu umelenga kufungua barabara ambapo ujenzi wa kivuko kwenye mto Kinshoka utazingatiwa awamu nyingine kadri bajeti itakavyoruhusu" alisema Kibona.

Kibona alisema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia sana kufungua mawasiliano na hivyo kurahisisha usafiri katika shughuli za kiuchumi na kijamii kati ya vijiji 6 vya Nselembwe, Tintigulu, Wembere, Kibigiri, Ntwike na Shelui vya Kata ya Shelui na Ntwike vyenye jumla ya wakazi 14,933.

Alisema vijiji vyenye wakazi hao vinajishughulisha na shughuli za kilimo na ufugaji.

Kibona alitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya miundombinu ya barabara kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo mradi huo ni sehemu ya ongezeko hilo.

Waziri Ummy Mwalimu baada ya kupokea taarifa hiyo aliwasihi Watendaji Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kuomba fedha mwaka wa fedha 2021/2023 Serikali Kuu kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa daraja la Kinshoka ili kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo.

Mkazi wa Kijiji hicho Neema Mathayo aliishukuru Serikali kwa kuwajengea barabara hiyo ambayo itakuwa ni mkombozi kwao kwa kuwa walikuwa na changamoto kubwa ya kupata usafiri wa kwenda kwenye shughuli zao za kiuchumi hasa wanawake wakati wa kwenda Hositali kwa ajili ya kujifungua.

Katika ziara hiyo Waziri Ummy alikagua barabara hiyo, ujenzi wa madarasa kupitia fedha za Uviko 19, mradi wa ujasiriamali wa Wasichana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kisiriri ambapo pia alizungunguza na Watumishi wa Halmashauri ya wilaya hiyo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.