• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERUKAMBA AFANYA ZIARA VIJIJI 15 KWA SIKU MOJA WILAYANI IKUNGI

Posted on: November 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, leo Novemba 16, 2023 amefanya ziara katika Wilaya ya Ikungi kwa lengo la kukagua na kutembelea miradi ya Maendeleo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake kwa kukutana na wananchi kupitia mikutano ya hadhara kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili.

Ziara hiyo yenye umbali wa zaidi ya Kilomita 400 kwenda na kurudi kutokea makao makuu ya Mkoa, mjini Singida ilihusisha baadhi ya vijiji kikiwemo cha Iyumbu, Makungu, Magungumka, Ufana, Mwankalaja, Kaugeli, Mdughuyu, Mlandala, Mpugizi, Mwaru, Maghonda, Mghungira na Ighombwe.

Akiwa katika kijiji cha Iyumbu kilichopo mpakani mwa Mkoa wa Tabora na Singida, Serukamba alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kata hiyo fedha za ujenzi wa shule mpya ya Sekondari inayogharimu Sh. Milioni 540/=.

Aidha, licha ya kupokea kero mbalimbali katika kijiji na Kata ya Iyumbu, Mkuu huyo wa Mkoa aliitaka idara ya ardhi Wilayani Ikungi kuhakikisha inatatua mgogoro wa mashamba pamoja na kuyapima maeneo hayo ili kuwapatia wakulima hati miliki.

Pia Serukamba alimtaka Afisa Kilimo wa Wilaya hiyo, Gulisha Msemo, kusimamia zoezi la upatikanaji wa mbolea ya ruzuku hadi kufikia Novemba 20, mwaka huu iwe imewafikia wakulima wote wanaohitaji.

Akiwa kijiji cha Makungu, Kata ya Iyumbu licha ya kuitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo kutenga Sh. Milioni Tatu (3,000,000/=) za ujenzi wa miundombinu ya kuvuna maji ya mvua kwa matumizi ya wanafunzi kupata huduma ya choo. Hata hivyo aliitaka RUWASA kumaliza kero ya maji katika kijiji hicho kwa kuchimba kisima kwa ushiriakiano wa Bonde la Kati na Halmashauri ya Wilaya.

Pamoja na kero ya maji kuonekana kuwa changamoto katika ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa aliiagiza RUWASA, kusimamia zoezi hilo ili kuwaondolea Wananchi adha ya maji, huku pia akihimiza upatikanaji wa mbolea kwa matumizi ya msimu mpya wa kilimo mwaka huu (2023/2024).

Kuhusu mradi wa REA unaoendelea kwenye maeneo mbalimbali Wilayani Ikungi, Serukamba alimwagiza Wakala wa Nishati Vijijini, kusimamia Wakandarasi ili ifikapo Desemba 31, mwaka huu Vijiji vyote vya Wilaya hiyo viwe vimefikiwa na nishati hiyo.

Katika ziara hiyo, Serukamba alifanikiwa kufika kwenye kambi ya wavuvi iliyopo katika kijiji cha Ufana Kata ya Mghungira, walioathiriwa na tukio la baadhi yao nyumba zao kuteketea kwa moto uliyosababisha mtu mmoja kupoteza uhai, na baada ya kuwapa faraja aliwataka kuchukua tahadhari dhidi ya majanga hayo ili kulinda mali na maisha yao.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa, aliwapongeza Wananchi wa kijiji cha Magungumka kwa kutumia nguvu na rasilimali zao kujenga na kupaua jengo la kituo kidogo cha Polisi ambapo alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, kuunga mkono juhudi hizo kwa kuhakikisha kituo hicho kinakamilika na kuanza kutoa huduma haraka.

Kuhusu ujenzi wa miradi ya afya na elimu, Serukamba alipongeza juhudi za Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, kwa kusimamia vyema ujenzi wa Zahanati mbalimbali zilizokamilika na kuanza kutoa huduma na akamuagiza Mkurugenzi kupeleka Wataalamu wa huduma za afya ili Wananchi waanze kunufaika na matunda ya Serikali yao.

Akizungumzia Sekta ya Elimu, Mkuu wa Mkoa huyo aliitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo kuunga mkono juhudi za Wananchi pale ambapo wameweza kuanzisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kupitia shule shikizi ili baadaye ziweze kupandishwa hadhi kwa kusajiliwa kuwa shule kamili.

Aidha katika ziara hiyo Wananchi wamemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa kwa kufanya uwamuzi wake wa kwenda kila kijiji ambapo amekuwa na utaratibu wa kukutana na Wananchi moja kwa moja kwa kuwafuata vijijini ili kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

http://singidars.blogspot.com/2023/11/serukamba-afanya-ziara-vijiji-15-kwa.html

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.