• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERUKAMBA AWAELEZA WALIMU NIA YA KUONDOA DARAJA SIFURI MKOANI SINGID

Posted on: January 16th, 2023

Walimu wa shule za Serikali Mkoani Singida wametakiwa kuhakikisha wanafuta daraja la sifuri na daraja la nne kwa kufanya kazi kwa bidii, kuwashirikisha wazazi na wanafunzi wenyewe.

Akiongea katika kikao kazi kilichowakutanisha Walimu wa shule za msingi, sekondari na wadhibiti ubora uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa RC Mission uliopo mjini Singida.

RC Serukamba amesema uondoaji wa madaraja hayo ya elimu utawezekana kwa kuacha uzembe, kuwahi kazini na kuwa na tabia ya kupata mrejesho baada ya kufundisha huku akiwataka wazazi kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula mashuleni.

Hata hivyo amewataka Maafisa elimu wa kata kuhakikisha wanatembelea mashule na kuhakikisha kila mwalimu anatimiza majukumu yake huku akiwakumbusha wadhibiti ubora kutowadhibiti walimu pekee badala yake waangalie changamoto zinazo wakabili walimu.

Aidha amewakumbusha walimu kahakikisha kwamba katika Mkoa wa Singida hakutakuwa na  Mwanafunzi atakayemaliza darasa la Saba bila kujua kusoma na kuandika.

Katika kuboresha Elimu RC Serukamba ameeleza nia yake ya kutaka kuanzisha mashindano kwa Shule za Sekondari ambapo shule ambayo haitapata daraja sifuri na daraja la nne watapata zawadi itakayo gawanywa kwa walimu wote wa shule husika.

"Umefika wakati sasa wadhibiti ubora kuhakikisha tunapata elimu bora kwa kuwa Serikali imeshawekeza vya kutosha katika majengo na miundombinu ya shule, umefika wakati Serikali kuwekeza katika ujuzi ili kuleta ubobezi katika masomo yanayofundisha" alieleza RC Serukamba.

Hata hivyo amewataka walimu kuendeleza juhudi na utamaduni wa kusoma vitabu badala ya kutumia mitandao ya kijamii.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko amesema Mkoa una jumla ya Walimu 7492 ambapo wa shule ya msingi ni 5166 na Sekondari ni Walimu 2326.

Amesema uwepo wa walimu hao kumesababisha kuanza kuboresha elimu ambapo amesema  kwa kidato cha sita ambapo ufaulu umefikia daraja la kwanza na kwa wanafunzi wa darasa la nne ameeleza kwamba waliofanya mtihani ni asilimia 93 na waliofaulu ni asilimia 82.

Hata hivyo RAS amesema katika zoezi la kuboresha elimu mkoani hapo tayari wameanzisha mkakati maalum ambapo utaboresha mahudhurio ya Walimu na Wanafunzi, ujenzi wa miundombinu na kuboresha uwajibikaji.

Aidha Mwaluko amesema tayari wameshaanza mafunzo ya Walimu ambapo jumla ya Walimu 1972 kati ya 7000 wameaanza kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Elimu ya Awali na Msingi TAMISEMI Suzan Nusu ameagiza kuendelea kutolewa kwa Mafunzo endelevu ya walimu kazini (Mewaka) ndani ya shule ili kujengeana uwezo na kuboresha Elimu na ufundishaji.

Mkutano huo ulihudhuriwa na jumla ya walimu 1956 kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Singida na kuhusisha walimu wa shule ya msingi, sekondari, Tume ya Utumishi wa walimu na wadhibiti ubora.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.