• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SIDO WATOE MAFUNZO KWA WANAFUNZI WA VYUO ILI WAJIAJIRI; RC NCHIMBI.

Posted on: October 17th, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amelitaka shirika la Viwanda Vidogo vidogo (SIDO) kuandaa mafunzo ya ujasiriamali kwa wanafunzi wa vyuo mbali mbali mkoani hapa ili wakihitimu waweze kujiajiri. 

Dkt. Nchimbi ametoa wito huo wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mikopo ya SIDO kwa wajasiriamali iliyofanyika kwenye viwanja vya SIDO ambapo amesema mafunzo hayo yatawajengea mazingira mazuri wahitimu kujiajiri. 

Amesema Mkoa wa Singida una fursa nyingi za kujiajiri pamoja na kuwa na vijana wengi hasa walipo katika vyuo mbalimbali lakini hawawekezi katika fursa hizo kwa kutokujua au kukosa elimu ya kutosha juu ya ujasiriamali, na hata waliopo vyuoni wakihitimu wanasubiri kuajiriwa badala ya kujiajiri. 

Dkt. Nchimbi amesema ili wananchi wakiwemo vijana waweze kuzitambua fursa hizo, SIDO Mkoa na wadau wengine wanapaswa kuongeza juhudi zaidi katika utoaji mafunzo ya ujasiriamali ambapo amewataka wajielekeze kwenye vyuo mbalimbali. 

“Singida ina kila aina ya fursa ambazo zinaweza kumkomboa mwananchi kiuchumi. Kwa hiyo hakuna sababu vijana au watu wengine kuukimbia mkoa wao na kwenda kutafuta maisha katika mikoa mingine. Ni suala la kujipanga na kupata fursa ya mafunzo kutoka SIDO mkoa”, amefafanua. 

Aidha ameziagiza halmashauri zote na manispaa Mkoani hapa kutangaza fursa, bidhaa, mazao, na huduma zinazopatikana katika maeneo yao ili kuwasaidia wajasiriamali kupata soko la uhakika.

 “ Halmashauri zote tumieni fedha mnazopata kwenye vyanzo vya mapato ya ndani  muwasaidie wajasiriamali wenu kutangaza kwenye vyombo vya habari, nina imani na uhakika kuwa mkitangaza bidhaa na mazao yao yatapata soko na nyinyi halmashauri mtapata mapato yenu”, amesema Dk.Nchimbi.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa SIDO Taifa Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji amesema SIDO imekuwa tegemeo kubwa kwa wajasiriamali hasa katika kutoa mafunzo na kusaidia teknolojia ya kuongeza thamani ya mazao na malighafi. 

“Mikopo ya SIDO imeweza kuwasaidia wajasiriamali kuthubutu na kuanzisha miradi ya usindikaji mara tu baada ya kupata mafunzo. Kundi hili limekuwa na changamoto ya mitaji kwa kuwa halikidhi na halijaweza kuthubutu kuzifikia benki kutokana na woga na gharama za mikopo”, amesema. 

Mhandisi Profesa Mpanduji amesema kwa kipindi cha mwaka 2016/2017 SIDO imeweza kutoa mikopo 4,464 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 7.2. Mikopo hiyo imetengeneza ajira 11,861 kati ya ajira hizo asilimia 51 ni wanawake. 

Kwa upande wake Meneja wa SIDO Mkoa wa Singida Shoma Kibende amesema kwa Mkoa wa Singida wametoa mikopo yenye jumla ya shilingi milioni 724.6 kwa wajasiriamali 693 na vikundi 47. Hali ya urejeshaji wa mikopo hiyo ni asilimia 98.

Kibende amesema SIDO wameweza kutoa mafunzo ya wajasiriamali mbalimbali 37 kwa wajasiriamali 996 ambao kati yao wanawake walikuwa 536 na wanaume 460. 

Amesema baadhi ya changamoto zinazowakabili kuwa ni upungufu wa wafanyakazi na ukosefu wa fedha kwa ajili ya kutekeleza mipango waliyojiwekea ikiwemo kuendeleza na kuboresha mtaa wa viwanda.

Naye Mjasiriamali kutoka Kampuni ya Singida Super Quality Oil and Rice mills Simon Kitundu amezishauri halmashauri na manispaa kutenga maeneo maalum ya kufanyia biashara wajasiriamali waweze kuondokana na adha mbalimbali ikiwemo ya kuuza bidhaa zao kwenye madirisha ya mabasi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.