• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA KUKABILIANA NA TATIZO LA MAFUTA YA KULA NCHINI

Posted on: August 8th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, amesema kuwa Singida imejikita katika kilimo cha alizeti ili kuhakikisha inazalisha kwa wingi mafuta ya kula yanayotokana na zao la alizeti kwa lengo la kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi.

Mkuu huyo ametoa maelezo hayo leo (tarehe 8 Agosti, 2023) wakati wa kilele cha maadhimisho ya maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Uvuvi yaliyohitimishwa Kanda ya Kati katika viwanja vya Nzuguni Jinini Dodoma.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida umejipanga katika kilimo cha mazao ya kimkakati ikiwemo kilimo cha zao hilo lengo kubwa likiwa ni kuhakikisha Mkoa huo unakuwa na mafuta ya kutosha kwa soko la ndani na nje hatua hiyo itakuwa imepunguza kwa kiasi kikubwa gharama ya uagizaji wa mafuta hayo kutoka nje ya nchi.

“Mkoa wa Singida unategemea kilimo kwa asilimia 80 na wakazi wake wamekuwa wakijikita zaidi katika kilimo na kwa maana hiyo tunahitaji kuwa na kilimo cha kimkakati ambacho kitaweza kuwainuwa wakulima kiuchumi kwa kuwaongezea kipato wao wenyewe na taifa kwa ujumla” ameeleza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha amesema kuwa Singida na Dodoma wamejipanga kufanya kilimo chenye tija ambacho kitaifanya mikoa ya Singida na Dodoma kuwa kitovu cha chakula nchini kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji katika skimu ya umwagiliaji zilizopo jambo ambalo litanyanyua uchumi wa Mkulima mmoja moja na taifa kwa ujumla wake.

Hata hivyo Serukamba amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassani kwa kuwekeza nguvu nyingi kwenye kilimo kwa maana ya kutoa pesa nyingi ambazo zitasaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji pamoja na kuwekeza katika uboreshaji wa pembejeo za kilimo, mifugo kwa njia ya uboreshaji wa majosho.

Amesema kitendo cha Rais Dk. Samia kuwekeza katika kilimo kitasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kusababisha kuwepo kwa mtawanyiko wa mvua ambazo hazieleweki.

“Kutokana na juhudi kubwa za Rais wa awamu ya sita kwa kuona umuhimu wa kuwekeza pesa nyingi kwenye kilimo, Serikali ya Singida kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imejipanga kuhakikisha inalima kilimo chenye tija na siyo kilimo cha kujikimu”

“Hata hivyo niwashauri Mabalozi kuhakikisha wanahamasisha kwa kuwatafuta wawekezaji wakubwa kuja nchini na kujenga viwanda vikubwa vya alizeti kwa ajili ya kuongeza mnyororo wa thamani na kwa kufanya hivyo vitajengwa viwanda vingi vya kuzalisha mafuta hayo na kusababisha uwepo wa mafuta ya kutosha”amesema Serukamba.

Sambamba na hayo amewapongeza washiriki wa makongamano ya maadhimisho ya kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kushiriki semina na mafunzo mbalimbali ya kilimo cha Alizeti, Mtama na ufugaji wa Kuku pamoja na kutembelea mabanda mbalimbali kwa ajili ya kujifunza kilimo chenye tija na chenye kuwaletea manufaa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.