• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Singida kutatua Mgogoro wa mashamba ya korosho uliodumu kwa miaka mitatu

Posted on: April 23rd, 2022

Kamati zinazoshughulikia changamoto ya ugawaji wa mashamba ya korosho wilayani Manyoni zimepewa Siku Saba kuanza tarehe 25 April 2022  kugawa na kuwaonesha mashamba wakulima wa zao hilo lengo likiwa ni kuhakikisha ifikapo Octoba  2022 yawe yamekwisha safishwa na kilimo kimeanza.

Kauli hiyo imetolewa leo  na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.  Binilith Mahenge alipokutana na wakulima zaidi ya Mia na hamsini  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Manyoni waliokuwa wakilalamikia mchakato wa ugawaji wa mashamba kugubikwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kukosa mashamba kwa wakulima waliolipia, mashamba kutosafishwa wakati yalishalipiwa na bàadhi ya wakulima walilipa fedha kwa muda mrefu lakini hawajaoneshwa mashamba yao.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.  Binilith Mahenge akizungumza wakati wa kikao hicho

RC Mahenge ameagiza kamati hizo kutumia Siku Saba kuanzia Siku ya tarehe 25 April kutambua majina ya wote wanaotakiwa kupatiwa mashamba na kuanza kuwaonesha mashamba yao huku akisisitiza kwamba hakuna mtu atakayepoteza haki yake.

Aidha ameagiza kuandaliwa andiko na mihtasari ya mikutano inayofanyika ili kusaidia usimamizi wa mashamba hayo na kurahisisha ufuatiliaji wakati wanapokuja viongozi wapya.

RC Mahenge amesema utaandaliwa utaratibu mzuri wa mawasiliano baina yao na wenye mashamba ili kuondoa changamoto hizo ambazo zimedumu kwa miaka zaidi mitatu.

"Changamoto zote zilizotokea mpaka kusababisha migogoro katika ugawaji wa mashamba na kutuchelewesha  kwa miaka mitatu limesababishwa na ufuatiliaji na usimamizi mbaya uliofanywa na bàadhi ya Maafisa wa Serikali, lazima tutengeneze utaratibu mzuri utakaosaidia kuendeleza zao la korosho mkoani hapa" alibainisha Dk. Mahenge.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko akizungumza wakati wa kikao hicho.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko amesema wamedhamiria kuondoa changamoto zilizojitokeza na watahakikisha kwamba ifikapo Oktoba 2022 mashamba yote yatakuwa yamekamilika ili kuongeza uzalishaji wa Korosho na kuongeza mapato ya Wilaya hiyo na Mkoa kwa ujumla.

Hata hivyo RAS huyo amewataka wakulima  kuiamini timu inayoshughulikia matatizo ya  changamoto hizo na kutoa ushirikiano pale utakapohitajika ikiwemo ukaguzi wa nyaraka za malipo na mahitaji mengine.

Aidha kwa kuanza kubadisha utaratibu RAS akabadilisha Mratibu wa Awali na kumteua Bwana Lucas Mkuki Afisa kilimo  kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kuendeleza  uratibu wa ugawaji wa mashamba ambapo atafanya kazi kwa kushirikiana na kamati zitakazokuwepo.

 Akizungumza kwa niaba ya wakulima wengine Abdala Mbonde ameishukuru Serikali ya Mkoa kwa maamuzi yao ya kuhakikisha  changamoto zinatatuliwa na kilimo cha korosho kinaanza.

 

Mbonde ameshauri kamati itakayoundwa ihakikishe haki inatendeka ili wakulima hao waweze kuendelea na uwekezaji huo katika kilimo hicho kwalengo la kujikwamua kiuchumi.

Mkutano ukiendelea

http://singidars.blogspot.com/2022/04/singida-kutatua-mgogoro-wa-mashamba-ya.html


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.